Utawafunga mikaba katika viuno na kuwavalisha kofia zao. Hivi ndivyo utakavyowatakasa Haruni na wana wake kuwa makuhani. Hao watakuwa makuhani siku zote kwa ajili ya sharti la siku zote.
Atafanya ibada ya upatanisho kwa ajili ya Pahali Patakatifu Sana, kwa ajili ya hema la mukutano, mazabahu, makuhani, na kwa ajili ya jamii nzima ya Israeli.
Ataoga mwili wote katika maji, kisha atavaa nguo takatifu. Ataingia pahali pale akiwa amevaa nguo takatifu: koti la kitani na atavaa kapitula ya kitani na akiwa amevaa kanzu ya kitani na kujifunga mukaba wa kitani.
Ikiwa kuhani ambaye amepakwa mafuta ndiye aliyetenda zambi hata akawatia watu katika kosa, basi huyo atamutolea Yawe ngombe dume muchanga asiyekuwa na kilema akuwe sadaka kwa ajili ya zambi.