Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 16:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Yule mutu aliyepeleka yule beberu kwa Azazeli kwanza atafua nguo zake na kuoga ndipo atakapoweza kuingia ndani ya kambi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 16:26
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kugusa nyama fulanifulani kunamufanya mutu kuwa muchafu. Yeyote atakayegusa mizoga yao atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu akitwaa sehemu ya mizoga yake atakuwa muchafu mpaka magaribi na nguo zake zinapaswa kufuliwa.


Nyama wote wanaotembelea kwa vitanga vyao ingawa wana miguu mine, ni wachafu kwenu na yeyote atakayegusa muzoga wa nyama kama huyo atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote anayebeba muzoga atakuwa muchafu mpaka magaribi, naye atasafisha nguo zake. Hao ni wachafu kwenu.


Hao wote ni wachafu kwenu na yeyote atakayegusa mizoga yao, atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Ikiwa muzoga wa viumbe hao unaangukia kitu chochote, kikuwe ni kifaa cha mbao au nguo au ngozi au gunia au chombo chochote kinachotumiwa kwa kazi yoyote, chombo hicho kitakuwa kichafu mpaka magaribi. Kwa kukifanya kikuwe safi kinapaswa kusafishwa kwa maji.


Ikiwa nyama yeyote munayeruhusiwa kula, anakufa mwenyewe, yeyote atakayegusa muzoga wake, atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote akikula nyama ya muzoga huo atafua nguo yake na atakuwa muchafu mpaka magaribi. Na yeyote atakayebeba muzoga huo, atafua nguo zake, naye atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Huyo mutu atafua nguo zake, atanyoa nywele zake, na kuoga, naye atakuwa safi. Nyuma ya hayo atarudi ndani ya kambi, lakini atakaa inje ya hema lake kwa muda wa siku saba.


Mutu yeyote atakayegusa vitu hivyo, atakuwa muchafu na anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Lakini yule beberu aliyeangukiwa na kura kwa ajili ya Azazeli atatolewa mbele ya Yawe akiwa muzima. Kwa kufanya ibada ya upatanisho, kuhani atamwacha aende katika jangwa kwa Azazeli, kwa ajili ya zambi za jamii.


Mafuta ya sadaka kwa ajili ya zambi atayateketeza juu ya mazabahu.


Yule mutu atakayewateketeza atafua nguo zake na kuoga, ndipo atakapoweza kuingia katika kambi.


Atawapigia kura hao beberu wawili, kura moja kwa ajili ya Yawe na nyingine kwa ajili ya Azazeli.


Hili ni sharti la kufuata siku zote. Mutu atakayenyunyiza maji ya utakaso atafua nguo zake; naye atakayegusa maji hayo atakuwa muchafu mpaka magaribi.


kwa maana Sheria ya Musa haikuleta ukamilifu. Lakini sasa kumeletwa tumaini nzuri zaidi, na kwa njia ya tumaini hili tunaweza kumukaribia Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ