Ataoga mule katika Pahali Patakatifu na kuvaa nguo zake. Atatoka na kutolea sadaka yake ya kuteketezwa, na sadaka ya kuteketezwa ya watu wa Israeli, kwa kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote.
Haruni atatoa huyo ngombe dume kwa sadaka ya kuondoa zambi kwa ajili yake mwenyewe na kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na jamaa yake.