Atafanya vile vile siku ya saba ya mwezi huo, kwa ajili ya kila mutu aliyetenda zambi bila kukusudia au kwa kutokujua. Kwa njia hiyo mutaitakasa nyumba ya Yawe.
Hivyo atafanya ibada ya upatanisho kwa ajili ya Pahali Patakatifu kwa sababu ya uchafu, makosa na zambi zote za Waisraeli. Ndivyo atakavyofanya vilevile kwa ajili ya hema la mukutano linalokuwa kati ya watu hao wanaokuwa wachafu.
Haruni ataweka mikono yake juu ya kichwa cha huyo beberu muzima na kuungama juu yake zambi zote za watu wa Israeli, makosa yao yote na zambi zao zote; naye ataziweka zote juu ya kichwa cha yule mbuzi. Kisha atamwacha huyo beberu aende katika jangwa akipelekwa kule na mutu yeyote anayekuwa tayari.
Musa akamuchinja huyo ngombe, akatwaa damu akapakaa pembe za mazabahu pande zote kwa kidole chake kwa kuitakasa. Kisha akatwaa damu iliyobaki akaimwanga chini kwenye tako la mazabahu ambayo alitakasa kwa kuifanyia ibada ya upatanisho.
Ni nani anayeweza basi kuwahukumu? Hakuna hata mumoja! Maana Yesu Kristo ndiye aliyekufa, na zaidi ya hiyo, alifufuka, na sasa anakaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu, na yeye ndiye anayetuombea.
Ndiyo kusema, Mungu ndiye aliyekuwa akipatanisha watu wote na yeye mwenyewe kwa njia ya Kristo bila kuhesabu makosa yao. Yeye ametupatia ujumbe wa upatanisho.
Kwa njia ya Mwana wake alitaka kupatanisha ulimwengu muzima naye. Kwa njia ya damu ya Mwana wake iliyomwangika juu ya musalaba, Mungu ameleta amani, hivi akapatanisha vitu vyote naye mwenyewe, vinavyokuwa katika dunia na katika mbingu.
Ni kwa sababu hii anaweza kuwaokoa kabisa wao wanaokuja kwa Mungu kwa njia yake, kwa maana yeye anaishi siku zote kusudi akuwe mwombezi mbele ya Mungu.