Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 16:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Akamwambia: Umwambie ndugu yako Haruni asiingie katika Pahali Patakatifu nyuma ya pazia wakati usiokubaliwa. Asiingie pahali pale maana ndipo nitakapotokea katika wingu juu ya kiti cha rehema. Asipotii, atakufa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 16:2
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Chumba cha ndani, kilichoitwa Pahali Patakatifu Sana, kilijengwa katika sehemu ya nyuma ya nyumba. Kilikuwa kimejengwa kwa mbao za mierezi kutokea kwenye sakafu mpaka kwenye dari, na urefu wake ulikuwa metre tisa.


Kisha makuhani wakaliingiza Sanduku la Agano la Yawe kwa nafasi yake katika chumba cha ndani cha nyumba, ni kusema Pahali Patakatifu Sana, chini ya mabawa ya makerubi.


Nao makuhani walishindwa kutumika kwa sababu ya wingu lile, maana utukufu wa Yawe ulijaza nyumba ya Mungu.


Haruni atafanya upatanisho juu ya pembe za mazabahu hiyo mara moja kwa mwaka. Ataifanyia upatanisho kwa damu ya sadaka ya maondoleo ya zambi mara moja kila mwaka katika vizazi vyenu vyote, maana mazabahu hiyo ni takatifu kabisa kwangu, mimi Yawe.


Kusudi asikufe, ataleta ubani ule mbele ya Yawe na kuutia katika moto kusudi moshi wa ubani ule ufunike kifuniko cha Sanduku la Agano.


Hili ni sharti la kufuata siku zote. Linapaswa kufuatwa kwa kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili ya watu wa Israeli mara moja kila mwaka na kusamehewa zambi zao. Musa akafanya yote kama vile alivyoamuriwa na Yawe.


Siku ya kumi ya mwezi huu wa saba ni siku ya upatanisho. Siku hiyo ni siku ya kuwa na mukutano mutakatifu. Mutafunga kula na kutoa sadaka Yawe anazotolewa kwa moto.


Mutabaki kwenye mulango wa hema la mukutano usiku na muchana kwa muda wa siku saba, mukifanya mambo Yawe aliyoamuru, kama sivyo mutakufa. Ndivyo nilivyoamuriwa na Yawe.


Ujitenge na watu hawa, niwaangamize mara moja! Lakini wao wakajitupa uso mpaka chini.


Lakini wewe peke yako na wana wako mutafanya kazi zote za kikuhani kwa ajili ya mazabahu na vyote vinavyokuwa ndani ya pazia. Hayo ni mapaswa yenu, kwa sababu ninawapa zawadi ya ukuhani. Mutu yeyote asiyestahili atakayekaribia vyombo vya hema, atauawa.


Basi, kwa kuwaepusha wasipate kuuawa kwa kukaribia vyombo hivyo vitakatifu sana utafanya hivi: Haruni na wana wake wataingia na kumupangia kila mumoja wao mapaswa yake na kazi yake.


Wakati wa kuvunja kambi, Haruni na wana wake wataingia katika hema, na kushusha pazia linalokuwa mbele ya Sanduku la Agano, kisha walifunike kwa pazia hilo.


Na saa ile ile pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini. Inchi ikatetemeka, mawe makubwa yakapasuka,


Tumaini hili linasimamisha imara na kulinda mioyo yetu kama vile nanga inavyosimamisha mashua imara. Nalo linapita katika pazia na kuingia katika Pahali Patakatifu Sana.


Kuhani Mukubwa wa Wayuda anaingia katika Pahali Patakatifu Sana kila mwaka, akibeba damu ya nyama. Lakini Kristo hakuingia humo kusudi ajitoe mwenyewe sadaka mara nyingi.


Na nyuma ya pazia lililotenga kile chumba cha kwanza, kulikuwa chumba kingine kilichoitwa Pahali Patakatifu Sana.


Na juu ya lile sanduku kulikuwa sanamu mbili za makerubi zilizoonyesha utukufu wa Mungu. Mabawa yao yalikuwa yakinyooshwa juu ya kiti cha rehema. Lakini sasa si wakati wa kueleza mambo hayo yote moja kwa moja.


Hekalu likajaa moshi kutokana na utukufu wa Mungu na uwezo wake. Na hakuna mutu aliyeweza kuingia ndani ya hekalu mpaka yale mapigo yaliyoletwa na wale wamalaika saba yalipotimizwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ