Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 16:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Wakati Haruni anafanya ibada ya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe, jamaa yake na jamii nzima ya Israeli, kusikuwe hata mutu yeyote ndani ya hema la mukutano mpaka wakati atakapokuwa amemaliza na kutoka inje.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 16:17
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Haruni na wazao wake ndio waliokuwa wakitoa sadaka juu ya mazabahu ya sadaka za kuteketezwa kwa moto na vilevile juu ya mazabahu ya kufukizia ubani. Walifanya kazi zote zilizoelekea Pahali Patakatifu Sana kwa kuifanyia Israeli upatanisho. Haya yote waliyafanya kulingana na maagizo Musa, mutumishi wa Mungu aliyotoa.


Mutu yeyote asikuje pamoja nawe, wala asionekane popote kwenye mulima, wala kondoo au ngombe wasikulishwe karibu yake.


Sisi wote tumepotea kama kondoo, kila mumoja wetu ameelekea njia yake. Lakini Yawe alimubebesha azabu, ambayo sisi wenyewe tuliistahili.


Muda wa miaka saba mara makumi saba umewekwa kwa ajili ya watu wako na juu ya muji wako mutakatifu kwa kumaliza makosa, kukomesha zambi, kusamehe uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri juu ya maono na unabii na kupakaa mafuta katika Pahali Patakatifu Sana.


Hivyo atafanya ibada ya upatanisho kwa ajili ya Pahali Patakatifu kwa sababu ya uchafu, makosa na zambi zote za Waisraeli. Ndivyo atakavyofanya vilevile kwa ajili ya hema la mukutano linalokuwa kati ya watu hao wanaokuwa wachafu.


Kisha atatoka na kwenda kwenye mazabahu inayokuwa mbele ya Yawe na kufanya ibada ya upatanisho. Atatwaa sehemu ya damu ya yule ngombe dume na ya yule mbuzi na kupakaa pembe za mazabahu pande zote.


Kundi kubwa la watu walikuwa inje wakiomba saa ile Zakaria alipokuwa akichoma ubani.


“Hivi hakuna anayeweza kuokolewa kwa njia ya mutu mwingine yeyote, kwa maana katika dunia nzima hakuna jina lingine lolote watu walilopewa lenye uwezo wa kuwaokoa.”


Kwa maana kuna Mungu mumoja tu, na kuna mupatanishi mumoja tu kati ya Mungu na watu, ni yule mutu, Kristo Yesu,


Yeye ni kitambulisho cha mwangaza wa utukufu wa Mungu, kwa maana yeye ni mufano kamili pahali ya Mungu mwenyewe, na kwa uwezo wa neno lake analinda vitu vyote. Naye alipokwisha kuwatakasa watu toka katika zambi zao, aliikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo wote.


Lakini ni Kuhani Mukubwa peke yake ndiye aliyeingia katika kile chumba cha pili mara moja tu kila mwaka. Naye alipaswa kupeleka mule damu ya nyama anayotoa sadaka kwa ajili ya zambi zake mwenyewe na kwa ajili ya zambi watu walizofanya kwa kutokujua.


Kristo yeye mwenyewe alibeba mizigo ya zambi zetu ndani ya mwili wake alipoteswa juu ya musalaba, kusudi tupate kuachana na zambi kabisa na kuishi maisha ya haki. Kwa ajili ya mapigo yake ninyi muliponyeshwa.


Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ