Walawi 16:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200213 Kusudi asikufe, ataleta ubani ule mbele ya Yawe na kuutia katika moto kusudi moshi wa ubani ule ufunike kifuniko cha Sanduku la Agano. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Haruni na wana wake watavaa makapitula hizo kila mara wanapoingia katika hema la mukutano, au wanapokaribia kwenye mazabahu, kufanya kazi za makuhani katika Pahali Patakatifu. Kwa njia hiyo hawataonyesha uchi wao na kuwa na hatari ya kuuawa. Hilo ni sharti la kufuatwa siku zote kwa Haruni na wazao wake.
Kisha Haruni na wana wake kufunika Pahali Patakatifu pamoja na vyombo na vifaa vyake vyote, wakiwa tayari kuanza safari, watu wa ukoo wa Kohati watakuja na kuvibeba. Lakini wao, hawaruhusiwi kabisa kugusa vyombo hivyo vitakatifu, kusudi wasikufe. Hiyo ndiyo kazi ya ukoo wa Kohati kila wakati hema la mukutano linapohamishwa.