4 Kitanda chochote atakacholalia au atakachoikalia, kitakuwa kichafu.
Na hii ndiyo sheria juu ya uchafu huo: muda wote anapotokwa na usaha au usaha unapokuwa umezuiwa ndani yake, mutu yule ni muchafu.
Mutu yeyote atakayegusa kitanda cha mutu yule anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.
Musidanganyike: “Warafiki wabaya wanaharibu tabia nzuri za watu.”
Musishiriki katika matendo ya giza yasiyofaa, lakini muyafichue.
Kila kitu ni safi kwa watu wanaokuwa safi. Lakini hakuna chochote kinachokuwa safi kwa watu wachafu na wasiomwamini Mungu, kwa maana akili na zamiri zao zimekuwa chafu.