Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 15:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 Ndivyo mutakavyotenga Waisraeli na uchafu wao, kusudi wasikufe katika uchafu wao juu ya kuchafua hema langu linalokuwa kati yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 15:31
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kama ningalikusudia maovu ndani ya moyo, Yawe hangalinisikiliza.


Tena si hayo tu! Wamekufuru hekalu langu na kuvunja Sabato zangu.


Wewe mwanadamu! Waisraeli walipoishi katika inchi yao waliichafua kwa mienendo na matendo yao. Niliyaona matendo yao kuwa sawa na mwanamuke anayekuwa muchafu wakati wa ugonjwa wake wa mwezi.


Makuhani watafundisha taifa langu kupambanua vitu vinavyokuwa vitakatifu na visivyokuwa vitakatifu, na kuwajulisha tofauti kati ya vitu vinavyokuwa vichafu na visivyokuwa vichafu.


Kwa hiyo, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– kwa vile mumechafua Pahali Patakatifu pangu, kwa matendo yenu mabaya na machukizo yenu, mimi nitawaangamiza bila huruma na bila kumwacha mutu yeyote.


Mutawala huyo atafanya mapatano imara na watu wengi kwa muda wa miaka saba. Kisha nusu ya muda huo atakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine. Pahali pa juu katika hekalu patasimamishwa chukizo linaloleta uharibifu, nalo litabaki pale mpaka yule aliyemusimamisha atakapoangamizwa kama ilivyopangwa na Mungu.


kwa kutia tofauti kati ya kisichokuwa kichafu na kinachokuwa kichafu, kinachoweza kukuliwa na kisichoweza kukuliwa.


Hiyo ni sheria juu ya taka la ukoma linalotokea katika nguo ya sufu au kitani au iliyofumwa au iliyosokotwa au ya ngozi. Kwa njia hiyo mutaweza kutia tofauti kati ya nguo isiyokuwa chafu na ile inayokuwa chafu.


Hiyo ndiyo sheria juu ya mwanaume anayetokwa na usaha na anayetokwa na mbegu za uzazi na kuwa muchafu.


Mutashika Sabato zangu na kuheshimu Pahali pangu Patakatifu. Mimi ni Yawe.


Mimi mwenyewe nitamukasirikia mutu huyu na kumutenga na watu wake kwa sababu alimutoa mumoja wa watoto wake sadaka kwa mungu Moleki na hivyo akachafua Pahali pangu Patakatifu na jina langu takatifu.


Lakini asilikaribie lile pazia wala ile mazabahu maana ana kilema, asipate kuchafua Pahali Patakatifu, kwa sababu mimi Yawe ndiye ninayewatakasa.


Anayegusa maiti, ni kusema mwili wa mutu aliyekufa, asipojitakasa, anachafua hema la Yawe, naye atatengwa na watu wa Israeli. Mutu huyo atabaki muchafu kwa sababu hakunyunyiziwa yale maji ya utakaso.


Lakini mutu muchafu asipojitakasa, mutu huyo atatengwa mbali na jamii, kwa sababu anachafua hema la Yawe. Kwa vile hakunyunyiziwa maji ya utakaso, yuko muchafu.


Mutawatoa inje ya kambi watu wote hawa, wanaume na wanawake, kusudi wasichafue kambi yangu ninamokaa.


Basi mutu akiharibu hekalu la Mungu, Mungu atamuharibu vilevile. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, na ninyi ndilo hekalu lake.


“Kama mutu akishikwa na ukoma munapaswa kuwa waangalifu kufuata maagizo ya Walawi. Kama vile nilivyowaamuru ndivyo mutakavyofuata kwa uangalifu.


Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?


Maana kuna watu wasiomuheshimu Mungu waliojiingiza kwa siri kati yetu. Watu hawa wanapotosha ujumbe wa neema ya Mungu wetu kusudi wapate kufanya uasherati na kumukana Yesu Kristo, anayekuwa peke yake Kiongozi na Bwana wetu. Tangia zamani Maandiko Matakatifu yamejulisha hukumu ile itakayowapata watu hawa.


Kwa hiyo ninaapa juu ya jamaa ya Eli kwamba uovu wao hautaondolewa hata kidogo kwa matoleo wala kwa sadaka.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ