Uwaambie watu wa Israeli hivi: Mwanamuke akipata mimba na kuzaa mutoto mwanaume, atakuwa muchafu kwa muda wa siku saba sawa vile anavyokuwa kwa wakati wake wa ugonjwa wa mwezi.
Kama mwanamuke anatokwa na damu kwa muda wa siku nyingi kuliko vile inavyokuwa kawaida au anatokwa damu wakati usiokuwa wa kawaida yake ya kutokwa damu, basi, ataendelea kuwa muchafu muda wote damu inapomutoka.