23 Mwanaume yeyote atakayegusa kitu chochote mwanamuke yule alicholalia au kuikalia, atakuwa muchafu mpaka magaribi.
Kugusa nyama fulanifulani kunamufanya mutu kuwa muchafu. Yeyote atakayegusa mizoga yao atakuwa muchafu mpaka magaribi.
Mutu yeyote atakayegusa kitu chochote mwanamuke huyo anachoikalia anapaswa kufua nguo zake na kuoga kwa maji, naye atakuwa muchafu mupaka magaribi.
Kama mwanaume akilala na mwanamuke huyo na damu ya huyo mwanamuke ikimudondokea huyo mwanaume, basi, mwanaume huyo atakuwa muchafu kwa muda wa siku saba. Kitanda chochote huyu mwanaume atakacholalia kitakuwa kichafu.
Chochote mutu muchafu atakachogusa kitakuwa kichafu, na yeyote atakayekigusa kitu hicho atakuwa muchafu mpaka magaribi.