Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 15:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Mwanaume yeyote akitokwa na mbegu za uzazi, anapaswa kuoga mwili muzima kwa maji, naye atakuwa muchafu mpaka magaribi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 15:16
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nguo yoyote iliyodondokewa mbegu za uzazi au ngozi yoyote iliyoguswa na mbegu zile inapaswa kusafishwa kwa maji na itakuwa chafu mpaka magaribi.


Kama mwanaume akilala na mwanamuke na kutokwa na mbegu za uzazi, basi, ni lazima wote wawili waoge kwa maji, nao watakuwa wachafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote atakayegusa kitanda cha mutu yule anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote wa kizazi cha Haruni akiwa na ugonjwa wa ukoma au anatokwa usaha asikule vitu vitakatifu mpaka atakapokuwa safi. Mutu yeyote akigusa mutu aliyejichafua kwa kugusa maiti au mutu aliyetokwa na mbegu za uzazi,


Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.


Lakini ikifika magaribi ataoga, na jua likitua anaweza kurudi katika kambi.


Wapendwa wangu, ninawasihi ninyi, kama vile wageni na wasafiri hapa katika dunia, muepuke tamaa za mwili zinazopigana na roho.


Lakini kama tunaishi katika mwangaza kama vile Mungu mwenyewe anavyokaa katika mwangaza, tunashirikiana sisi kwa sisi, na damu ya Mwana wake Yesu inasafisha zambi zetu zote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ