Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 15:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Mwanaume yeyote anayetokwa na usaha akiponywa ugonjwa wake, mutu yule anapaswa kungoja siku saba mbele ya kuondolewa uchafu wake. Atafua nguo zake na kuoga kwa maji ya muto, naye atakuwa safi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 15:13
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hivi ndivyo utakavyowatendea Haruni na wana wake kufuatana na yote yale niliyokuamuru. Utawatakasa kwa muda wa siku saba,


Kwa siku saba utafanyia mazabahu upatanisho na kuitakasa. Nyuma ya hayo, mazabahu itakuwa takatifu kabisa na chochote kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.


Nitatakasa zambi zao zote na kuwasamehe uovu wao na uasi walionitendea.


Siku ya nane ataleta wana-kondoo dume wawili wasiokuwa na kilema, kondoo dike wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema, kilo tatu za unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya vyakula pamoja na mafuta sehemu moja ya tatu ya litre.


Huyo mutu atafua nguo zake, atanyoa nywele zake, na kuoga, naye atakuwa safi. Nyuma ya hayo atarudi ndani ya kambi, lakini atakaa inje ya hema lake kwa muda wa siku saba.


Nyuma ya kukauka damu yake mwanamuke huyo atangoja bado siku saba kwa kuwa safi, na nyuma ya muda ule atakuwa safi.


Mutu yeyote atakayegusa kitanda cha mutu yule anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Hamutatoka inje ya mulango wa hema la mukutano kwa muda wote wa siku saba, ni kusema mpaka muda wenu wa kutakaswa umekwisha, muda ambao utatwaa siku saba.


Siku ya nane kisha siku saba za kutakaswa, Musa akamwita Haruni na wana wake pamoja na wazee wa Israeli.


Lakini Yawe akamwambia Musa: Kama baba yake angemutemea mate kwenye uso, basi, hangepata haya kwa siku saba? Basi, umutoe inje ya kambi akae kule muda wa siku saba, kisha unaweza kumuruhusu arudi katika kambi.


Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.


Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia. Musafishe mikono yenu, ninyi wenye zambi! Mutakase mioyo yenu, ninyi wenye nia mbili!


na kutoka kwa Yesu Kristo. Yeye ni mushuhuda mwaminifu, naye ndiye wa kwanza aliyefufuliwa, vilevile yeye ni mukubwa wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda na ametukomboa toka katika zambi zetu kwa njia ya damu yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ