11 Mutu yeyote anayetokwa na usaha akimugusa mutu bila kusafisha kwanza mikono yake na kuoga, aliyeguswa atakuwa muchafu mpaka magaribi.
Kugusa nyama fulanifulani kunamufanya mutu kuwa muchafu. Yeyote atakayegusa mizoga yao atakuwa muchafu mpaka magaribi.
Mutu yeyote atakayegusa kitu chochote mutu huyu alichoikalia atakuwa muchafu mpaka magaribi. Mutu yeyote anayebeba kitu chochote kilichokuwa cha mutu huyu anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.
Chombo chochote cha udongo kilichoguswa na mutu anayetokwa na usaha kinapaswa kuvunjwa. Lakini chombo chochote cha mbao kitasafishwa kwa maji.
Chochote mutu muchafu atakachogusa kitakuwa kichafu, na yeyote atakayekigusa kitu hicho atakuwa muchafu mpaka magaribi.
Kama kati yenu kuna mutu yeyote ambaye ni muchafu kwa sababu ya kutokwa mbegu usiku, huyo atatoka inje ya kambi; hatakaa karibu na kambi.