Kuhani atatolea ile sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya vyakula juu ya mazabahu. Hivyo kuhani atamufanyia yule mutu ibada ya upatanisho, naye atakuwa safi.
Huyo mutu atafua nguo zake, atanyoa nywele zake, na kuoga, naye atakuwa safi. Nyuma ya hayo atarudi ndani ya kambi, lakini atakaa inje ya hema lake kwa muda wa siku saba.
Kama mutu anakufa kwa rafla karibu na munaziri na kuchafua nywele zake, huyu munaziri atanyoa kichwa chake wakati wa siku ya kutakaswa kwake; atakinyoa katika siku ya saba.