Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 14:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Huyo mutu atafua nguo zake, atanyoa nywele zake, na kuoga, naye atakuwa safi. Nyuma ya hayo atarudi ndani ya kambi, lakini atakaa inje ya hema lake kwa muda wa siku saba.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 14:8
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi mufalme Uzia akakuwa na ukoma mpaka siku ya kufa kwake. Alikaa katika nyumba yake ya pekee maana hakukubaliwa tena kuingia katika nyumba ya Yawe. Na Yotamu mutoto wake, akatunza jamaa yake akitawala wakaaji wa inchi.


Yawe akamwambia Musa: “Kwenda kwa watu uwatakase leo na kesho. Uwaambie wafue nguo zao


Basi, Musa akashuka toka juu ya mulima na kuwaendea watu, akawatakasa, nao wakafua nguo zao.


Mutu akitwaa sehemu ya mizoga yake atakuwa muchafu mpaka magaribi na nguo zake zinapaswa kufuliwa.


Kuhani atatolea ile sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya vyakula juu ya mazabahu. Hivyo kuhani atamufanyia yule mutu ibada ya upatanisho, naye atakuwa safi.


Siku ya saba atanyoa nywele zake zote, ndevu na kope za macho yake. Kisha atafua nguo zake na kuoga, ataoga kwa maji, naye atakuwa safi.


Mwanaume yeyote anayetokwa na usaha akiponywa ugonjwa wake, mutu yule anapaswa kungoja siku saba mbele ya kuondolewa uchafu wake. Atafua nguo zake na kuoga kwa maji ya muto, naye atakuwa safi.


Halafu Musa akawaleta Haruni na wana wake na kuwanawisha.


Kama mutu anakufa kwa rafla karibu na munaziri na kuchafua nywele zake, huyu munaziri atanyoa kichwa chake wakati wa siku ya kutakaswa kwake; atakinyoa katika siku ya saba.


Hivi ndivyo utakavyowatakasa: uwanyunyizie maji ya utakaso kisha uwaambie wajinyoe mwili muzima, wafue nguo zao na kujitakasa.


basi, anaweza kumupeleka kwake. Yule mwanamuke atanyoa kichwa chake na kukata kucha zake,


Maji haya ni mufano wa ubatizo unaowaokoa ninyi sasa. Ubatizo ule si kwa ajili ya kusafisha uchafu wa mwili lakini ni njia ya kufanya mapatano na Mungu katika zamiri safi. Nao unawaokoa ninyi kwa njia ya ufufuko wa Yesu Kristo,


Nami nikamujibu: “Bwana wangu wewe ndiwe unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wanaotoka katika mateso makubwa. Wamesafisha kanzu zao na kuzifanya kuwa nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ