Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 14:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kisha, atamunyunyizia yule mwenye kutakaswa ile damu mara saba, halafu atamutangaza mutu huyo kuwa safi. Atamwacha yule ndege muzima aende zake katika pori inje ya muji.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 14:7
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Elisha akamutuma mutumishi wake amwambie: “Kwenda uoge mara saba katika muto Yordani, nawe utapona kabisa.”


Basi, Namani akateremuka kwenye muto Yordani akajitumbukiza mule mara saba, kama alivyoagizwa na Elisha mutu wa Mungu, naye akapona kabisa. Ngozi yake ikakuwa laini na yenye afya kama ya mutoto mudogo.


Mimi ni mukosaji tangia kuzaliwa kwangu, mwenye zambi tangia tumbo la mama yangu.


Lakini sasa ameyashangaza mataifa mengi. Wafalme watapumbazika kwa sababu yake, maana wataona mambo ambayo hawajapata kuambiwa, na kufahamu mambo ambayo hawajapata kusikia.


Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mutakuwa safi. Nitawatakasa toka uchafu wenu wote na toka uchafu wa sanamu za miungu yenu yote.


Muda wa miaka saba mara makumi saba umewekwa kwa ajili ya watu wako na juu ya muji wako mutakatifu kwa kumaliza makosa, kukomesha zambi, kusamehe uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri juu ya maono na unabii na kupakaa mafuta katika Pahali Patakatifu Sana.


pale kuhani atamwangalia. Kuhani akiona kwamba ukoma umemwenea mwili muzima, basi, atamutangaza mutu yule kuwa safi kwa sababu mwili umegeuka kuwa mweupe na hivyo mutu yule ni safi.


Kuhani atamwangalia na akiona kwamba kimegeuka kuwa cheupe, basi, atamutangaza mutu yule kuwa safi.


Atatwaa kipande cha mwerezi, tawi la hisopo na ile sufu nyekundu pamoja na yule ndege mwingine anayekuwa muzima na kuvitumbukiza vyote katika damu ya yule ndege aliyechinjwa. Kisha atanyunyizia nyumba hiyo damu mara saba.


Atatwaa sehemu ya damu ya yule ngombe dume na kunyunyiza kwa kidole chake upande wa mashariki juu ya kiti cha rehema kisha atainyunyizia mbele ya Sanduku la Agano mara saba kwa kidole chake.


Atainyunyizia mazabahu hiyo damu kwa kidole chake mara saba na hivyo ataisafisha na kuitakasa toka uchafu wote wa watu wa Israeli.


Atamwacha huyo beberu aende katika jangwa, pahali pasipokuwa watu, akiwa amebeba maovu yao yote.


Atachovya kidole chake katika hiyo damu na kuinyunyiza mbele ya pazia mara saba, mbele ya Yawe.


Atachovya kidole chake katika damu hiyo na kuinyunyiza mara saba mbele ya Yawe upande wa mbele wa pazia la Pahali Patakatifu.


Akanyunyiza sehemu ya mafuta hayo juu ya mazabahu mara saba, akaipakaa mafuta na vyombo vyake vyote, birika na tako lake kwa kuvitakasa.


Utatuhurumia tena; utatupilia mbali zambi zetu, utazitupa zote katika vilindi vya bahari.


Siku ya tatu na ya saba mutu huyo atajitakasa kwa yale maji ya utakaso, naye atakuwa safi. Lakini akiacha kujitakasa katika siku ya tatu na ya saba, mutu huyo atabaki muchafu.


Lakini askari mumoja akamuchoma mukuki katika ubavu; mara moja damu na maji vikatoka.


Basi tumwendee Mungu kwa moyo wa uaminifu, kwa imani kamilifu, kwa moyo uliosafishwa toka zamiri mbaya na mwili uliosafishwa na maji safi.


Mumefikia karibu na Yesu anayekuwa mupatanishi wa agano jipya, na kwenye damu yake iliyomwangwa inayosema nasi maneno mema zaidi kuliko damu ya Abeli.


Watu waliohesabiwa kuwa wachafu kufuatana na desturi, walitakaswa uchafu wao wa kimwili kwa njia ya kunyunyizwa damu ya mbuzi na ya ngombe pamoja na majivu ya ngombe aliyeteketezwa kwa moto.


Kwa maana, kwanza Musa aliwatangazia watu wote amri zote za Sheria. Kisha akatwaa damu ya ngombe pamoja na maji, naye akavinyunyiza juu ya kitabu cha Sheria na juu ya watu wote akitumia manyoya mekundu na vitawi vya muti wa hisopo.


Musa akanyunyiza vilevile damu juu ya Hema na juu ya vyombo vyote vya ibada.


Ingekuwa hivi, ingemupasa ateswe mara nyingi tangu kuumbwa kwa dunia. Lakini sasa, wakati ukikaribia kwa mwisho, yeye alitokea mara moja tu kusudi awasamehe watu zambi kwa njia ya kujitoa mwenyewe sadaka.


Mungu Baba aliwachagua ninyi tangu mbele kufuatana na mupango wake na kufanywa watakatifu na Roho, mupate kumutii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Ninawatakia neema na amani kwa uwingi.


Yesu Kristo ndiye aliyekuja kwa maji ya ubatizo wake na kwa damu ya kufa kwake. Hakukuja na maji tu, lakini pamoja na maji na damu. Naye Roho ndiye anayeshuhudia mambo yale kwa sababu Roho ni wa ukweli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ