Kuhani atachunguza pahali panapokuwa ugonjwa na ikiwa nywele za pahali pale zimebadilika kuwa nyeupe na ugonjwa wenyewe ukionekana kuwa uko ndani zaidi ya ngozi ya mwili wake, basi, huo ni ukoma. Kuhani akimaliza kumuchunguza, hivyo atatangaza kwamba mutu yule ni muchafu.
Unga huo utachanganywa na mafuta na kupikwa juu ya kikaango. Kisha utauleta ukiwa vipandevipande na kumutolea Yawe na harufu ya sadaka yake itamupendeza Mungu.
Basi, hii ndiyo sheria kuelekea sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya vyakula, sadaka kwa ajili ya zambi, sadaka kwa ajili ya kosa, kuelekea kutakaswa na kuelekea sadaka ya amani.
Na hii ndiyo sheria ya kufuatwa kama mutu akikufia ndani ya hema: Kila mutu atakayeingia ndani ya hema hilo, au aliyekuwa ndani ya hema hilo, atakuwa muchafu kwa siku saba.