Kuhani atatolea ile sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya vyakula juu ya mazabahu. Hivyo kuhani atamufanyia yule mutu ibada ya upatanisho, naye atakuwa safi.
Hivi ndivyo atakavyotakasa nyumba hiyo kwa damu ya ndege, maji safi ya chemichemi, ndege muzima, kipande cha muti wa mwerezi, tawi la hisopo na ile sufu nyekundu.
Kisha, atamunyunyizia yule mwenye kutakaswa ile damu mara saba, halafu atamutangaza mutu huyo kuwa safi. Atamwacha yule ndege muzima aende zake katika pori inje ya muji.