Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 14:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Mutakapoingia katika inchi ya Kanana ambayo ninawapa kuwa urizi wenu, nami nikifanya namna ya ukoma uote katika ukuta wa nyumba fulani katika inchi mutakayorizi,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 14:34
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yawe akamutokea Abramu, akamwambia: “Nitawapa wazao wako inchi hii.” Basi, Abramu akajenga mazabahu kwa ajili ya Yawe aliyemutokea.


Basi, simama uitembelee inchi hii katika upana na urefu, maana nitakupa wewe inchi ile.”


Nitakupa wewe na wazao wako inchi hii ambamo unaishi kama mugeni. Ni kusema inchi yote ya Kanana ikuwe mali yenu milele; nami nitakuwa Mungu wao.”


akawaambia: “Ikiwa mutaisikiliza kwa uaminifu sauti yangu mimi Yawe, Mungu wenu, kutenda yale yanayokuwa sawa mbele yangu, na kuheshimu amri na masharti yangu yote, basi, mimi sitawaletea yale magonjwa niliyowaletea Wamisri. Kwa sababu, mimi ni Yawe ninayewaponya ninyi.”


Yawe analaani nyumba za waovu, lakini anabariki makao ya wenye haki.


Mimi ninafanya mwangaza na kuumba giza; ninaleta uheri na kusababisha hasara. Mimi Yawe ninatenda vitu hivi vyote.


Lakini, nimekwisha kuwaambia: Mutarizi inchi yao, mimi ninawapa inchi hiyo ikuwe yenu, inchi inayotiririka maziwa na asali. Mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatenga na mataifa mengine.


Uwaambie Waisraeli hivi: Mutakapoingia katika inchi ambayo ninawapa na kuvuna mazao yake, mutamuletea kuhani muganda wa mavuno ya kwanza.


Uwaambie Waisraeli hivi: Mutakapofika katika inchi ninayowapa mimi Yawe, kila mwaka wa saba inchi itapumzishwa isilimwe kwa heshima ya Yawe.


Baragumu ya vita inalia katika muji bila kutia watu hofu? Muji unaweza kupatwa na hasara ambayo haikuletwa na Mungu?


Yawe anatoa amri, na nyumba kubwa inabomoka vipandevipande, na nyumba ndogo kusagikasagika.


Yawe anawaita wakaaji wa muji, na ni jambo la hekima sana kumutii yeye: Musikilize, enyi watu wa Yuda; musikilize enyi muliokusanyika katika muji.


Yawe wa majeshi anasema kwamba yeye mwenyewe ataipeleka laana hiyo. Itapenya kila nyumba ya mwizi na kila nyumba ya mwenye kuapa uongo kwa kutumia jina lake; itakaa mule na kuteketeza nyumba hiyo yote, mbao na mawe.


na kurizi inchi. Mukisha kufanya hayo, mutarudi, maana mutakuwa bila kosa mbele ya Yawe na wandugu zenu Waisraeli. Kisha Yawe atakubali inchi hii ya upande wa mashariki wa Yordani kuwa mali yenu.


Chini ya uongozi wa Yawe, tutavuka na silaha zetu mpaka katika inchi ya Kanana, lakini inchi tuliyopewa hapa upande wa mashariki wa Yordani itakuwa mali yetu.


Uwaambie Waisraeli kwamba wakati mutakapovuka muto Yordani na kuingia katika inchi ya Kanana,


“Haya ndiyo masharti na maagizo ambayo mutatimiza katika inchi ambayo Yawe, Mungu wa babu zenu amewapa kwa kuirizi, siku zote za kuishi kwenu juu ya inchi.


“Wakati Yawe, Mungu wenu, atakapoteketeza watu wale ambao anawapa ninyi inchi yao, na kisha kuitwaa na kuishi katika nyumba zao,


“Na kisha kufika na kurizi inchi ambayo Yawe, Mungu wenu anawapa ikuwe yenu na kuishi huko,


Juu yake mutaandika maneno yote ya sheria hizi zote, mutakapoingia katika inchi ile inayotiririka maziwa na asali, ambayo Yawe, Mungu wa wazee wenu, aliwaahidi.


“Panda juu ya mulima huu wa Abarimu, mulima Nebo katika inchi ya Moabu, kuelekea muji wa Yeriko, uiangalie inchi ya Kanana ninayowapa Waisraeli wairizi.


Yawe atawaondolea magonjwa yote na hamutapatwa na magonjwa yoyote ya kutisha kama yaliyowapata huko Misri, lakini atawapa waadui zenu magonjwa hayo.


Wakati huu, Yoshua alikuwa muzee wa miaka mingi. Basi, Yawe akamwambia: “Wewe sasa umekuwa muzee wa miaka mingi, na kumebaki bado sehemu kubwa za inchi ambazo hazijatwaliwa.


Yawe anaua na kufufua, yeye anawashusha katika kuzimu naye anawarudisha tena.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ