Atachinja yule mwana-kondoo dume wa sadaka kwa ajili ya kosa. Kuhani atatwaa sehemu ya damu na kumupakaa yule mutu anayetakaswa katika incha ya sikio lake la kuume, katika kidole gumba cha mukono wake wa kuume na kidole gumba cha muguu wake wa kuume.
Kisha atamunyunyizia yule mutu kwa kidole cha mukono wake wa kuume sehemu ya hayo mafuta yanayokuwa katika kigaja chake cha kushoto mara saba mbele ya Yawe.