Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 14:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Lakini ikiwa mutu yule ni masikini, hana uwezo wa kutoa vitu hivyo, basi ataleta mwana-kondoo dume mumoja kuwa malipo ya sadaka kwa ajili ya kosa ambaye atafanyiwa kitambulisho cha kutoa sadaka kwa kumufanyia yule mutu ibada ya upatanisho. Ataleta vilevile kilo moja ya unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya vyakula na mafuta sehemu moja ya tatu ya litre.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 14:21
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yeye hawapendelei wakubwa, wala kuwajali watajiri kuliko wamasikini, maana wote hao ni kazi ya mikono yake.


Anayechekelea masikini anamutukana Muumba wake; anayefurahia hasara hatakosa kuazibiwa.


Watajiri na wamasikini wana hali hii moja: Yawe ni Muumba wao wote.


Pamoja na kila ngombe dume na kila kondoo dume anayetolewa sadaka, kunapaswa kuwa litre kumi na saba na nusu za unga, na pamoja na kila mwana-kondoo, kunapaswa kuwa chochote ambacho mufalme anatoa. Tena kwa kila sadaka ya unga, kunapaswa kutolewa litre tatu za unga.


Ikiwa anamutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa ya ndege, basi, ataleta sadaka yake ya hua au kitoto cha njiwa.


Kama hawezi kutoa mwana-kondoo, basi, ataleta hua wawili au vitoto viwili vya njiwa; mumoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya zambi. Kuhani atamufanyia mama huyo ibada ya upatanisho, naye atakuwa safi.


Siku ya nane ataleta wana-kondoo dume wawili wasiokuwa na kilema, kondoo dike wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema, kilo tatu za unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya vyakula pamoja na mafuta sehemu moja ya tatu ya litre.


Ataleta vilevile hua wawili au vitoto viwili vya njiwa kadiri anavyoweza mumoja atakuwa kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.


Lakini ikiwa mutu huyu ni masikini na hawezi kulipa malipo yake, basi, mutu yule atapelekwa kwa kuhani. Kuhani atapima bei yake kulingana na uwezo wa huyo aliyefanya kiapo.


Ikiwa hawezi kutoa hua wawili au vitoto viwili vya njiwa kama vile sadaka yake kwa ajili ya zambi aliyotenda, basi, ataleta unga kilo moja. Lakini hatautia mafuta wala ubani maana ni sadaka kwa ajili ya zambi.


Lakini kama hawezi kutoa mwana-kondoo wa sadaka ya kosa kwa ajili ya zambi aliyotenda, basi atamuletea Yawe hua wawili au vitoto viwili vya njiwa, mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa moto.


Kisha Yesu akawaangalia wanafunzi wake na kusema: “Heri kwenu munaokuwa wamasikini, maana Ufalme wa Mungu ni kwenu.


Kwa maana kama mutu akiwa na moyo wa kutoa, Mungu anakubali kitu anachotoa kufuatana na kile anachokuwa nacho, wala si kufuatana na kile asichokuwa nacho.


Kwa maana munajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, ingawa alikuwa tajiri, yeye mwenyewe alijifanya masikini kwa ajili yenu, kusudi mupate kuwa watajiri kwa njia ya umasikini wake.


Anawainua wazaifu toka katika mavumbi, anawanyanyua wakosefu toka katika majivu, na kuwaikalisha pamoja na wakubwa, na kuwarizisha viti vya heshima. Maana, minara ya dunia ni ya Yawe; yeye ameisimika dunia juu ya minara yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ