Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 14:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Kuhani atatwaa sehemu ya damu ya sadaka kwa ajili ya kosa na kumupakaa mutu anayetakaswa katika incha ya sikio lake la kuume na kidole gumba cha mukono wake wa kuume na kidole gumba cha muguu wake wa kuume.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 14:14
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nawe utamuchinja na kutwaa sehemu ya damu na kumupakaa Haruni na wana wake kwenye incha za masikio yao ya kuume na vidole gumba vya mikono yao ya kuume, na vidole gumba vya miguu yao ya kuume. Damu inayobaki utairushia juu ya mazabahu pande zake zote.


Niwapige wapi tena, ninyi munaoendelea kuasi? Kichwa chote kinajaa vidonda, na moyo unaumia kabisa!


Kuhani atatolea sadaka kwa ajili ya zambi na kumufanyia yule mutu anayetakaswa ibada ya upatanisho kwa kumwondolea uchafu wake. Kisha atachinja mwana-kondoo wa sadaka ya kuteketezwa.


Atachinja yule mwana-kondoo dume wa sadaka kwa ajili ya kosa. Kuhani atatwaa sehemu ya damu na kumupakaa yule mutu anayetakaswa katika incha ya sikio lake la kuume, katika kidole gumba cha mukono wake wa kuume na kidole gumba cha muguu wake wa kuume.


Basi wandugu zangu, kufuatana na vile Mungu alivyoonyesha huruma yake kwetu, ninawasihi mujitoe wenyewe kwake kuwa sadaka yenye uzima, takatifu na yenye kumupendeza. Hii ndiyo njia ya kweli ya kumwabudu.


Musitoe tena viungo vya mwili wenu kufanya zambi, mukivitumikisha kama vyombo vya kufanya mabaya. Lakini mujitoe wenyewe kwa kumutumikia Mungu kama watu waliofufuliwa na mutumikishe viungo vya mwili wenu kama vyombo vya kufanya haki.


(Ninatumia luga ya kawaida ya wanadamu kwa sababu ya uzaifu wenu wa kimutu). Zamani mulijitoa kabisa kuwa watumwa wa kufanya mambo machafu na maovu kwa kuishi katika machafuko. Hivi vilevile mujitoe kabisa kuwa watumwa wa kufanya haki kusudi muweze kuishi katika utakatifu.


Kwa sababu mulinunuliwa na Mungu kwa bei kali. Basi mutumie miili yenu na roho zenu kwa utukufu wa Mungu.


Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.


“Kama mutu akishikwa na ukoma munapaswa kuwa waangalifu kufuata maagizo ya Walawi. Kama vile nilivyowaamuru ndivyo mutakavyofuata kwa uangalifu.


Kwa maana kama vile ninavyongojea na kutumainia sana, sitafezeheka hata kidogo. Lakini tangia sasa na hata siku zote, nitamutukuza Kristo kwa uhodari katika maisha yangu, ikiwa nitaishi au nitakufa.


Nanyi vilevile, kama mawe yenye uzima mutumiwe kwa kujenga hekalu la kiroho. Na mule mutafanya kazi takatifu ya ukuhani kwa kutoa sadaka za kiroho zinazomupendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ