Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 14:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Siku ya nane ataleta wana-kondoo dume wawili wasiokuwa na kilema, kondoo dike wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema, kilo tatu za unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya vyakula pamoja na mafuta sehemu moja ya tatu ya litre.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 14:10
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Pamoja na mwana-kondoo wa kwanza, utatoa kilo moja ya unga laini uliochanganywa na litre moja ya mafuta safi, na litre moja ya divai kama sadaka ya kinywaji.


Kama sadaka yake ya kuteketezwa ataitwaa katika kundi la kondoo au mbuzi, basi atachagua dume asiyekuwa na kilema.


Kama sadaka mutu anayotoa ni ya kuteketezwa kwa moto, atamuchagua nyama dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake, atamutolea mbele ya mulango wa hema la mukutano kusudi apate kukubaliwa na Yawe;


Kuhani atakayetakasa mutu huyo atamuleta mbele ya Yawe karibu na mulango wa hema la mukutano pamoja na vitu alivyoleta.


Kuhani atatwaa mwana-kondoo dume mumoja na kumutolea sadaka kwa ajili ya kosa pamoja na yale mafuta sehemu moja ya tatu ya litre. Atafanya kitambulisho cha kuvitolea mbele ya Yawe.


Kisha, kuhani atatwaa sehemu ya ile sehemu moja ya tatu ya mafuta na kuyatia katika kigaja cha mukono wake wa kushoto.


Lakini ikiwa mutu yule ni masikini, hana uwezo wa kutoa vitu hivyo, basi ataleta mwana-kondoo dume mumoja kuwa malipo ya sadaka kwa ajili ya kosa ambaye atafanyiwa kitambulisho cha kutoa sadaka kwa kumufanyia yule mutu ibada ya upatanisho. Ataleta vilevile kilo moja ya unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya vyakula na mafuta sehemu moja ya tatu ya litre.


Mutu yeyote akileta sadaka ya ngano kwa Yawe, sadaka hiyo ikuwe ya unga laini. Atautia mafuta na ubani.


Sadaka yoyote ya ngano utakayomuletea Yawe inapaswa kuwa imetengenezwa bila chachu, maana hakuna ruhusa hata kidogo ya kutumia chachu wala asali katika sadaka Yawe anazotolewa kwa moto.


Utakoleza sadaka zako zote za ngano kwa chumvi. Usiache hata kidogo kuweka chumvi katika sadaka yako ya ngano, maana chumvi ni kitambulisho cha agano Mungu alilofanya pamoja nanyi.


Pamoja na sadaka hiyo, mutatoa sadaka ya vyakula ya kilo mbili za unga laini uliochanganywa na mafuta ambayo mutanitolea mimi Yawe kwa moto, na harufu yake itanipendeza. Sadaka yake ya kinywaji ni litre moja ya divai.


Ikiwa mutu yule ataleta mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya zambi, basi, ataleta mwana-kondoo dike asiyekuwa na kilema.


Siku ya nane kisha siku saba za kutakaswa, Musa akamwita Haruni na wana wake pamoja na wazee wa Israeli.


Sadaka ya ngano itakayoandamana nazo itakuwa ya unga safi uliochanganywa na mafuta, kilo tatu kwa kila ngombe dume, kilo mbili kwa kila kondoo dume,


na kumutolea Yawe zawadi zake: mwana-kondoo dume mumoja wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; mwana-kondoo dike mumoja wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya zambi; na kondoo dume mumoja asiyekuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya amani.


Kisha Yesu akamwambia: “Angalisho, usimwambie mutu neno juu ya hii. Lakini kwenda na kumwonyesha kuhani jinsi unavyokuwa sasa. Kisha utoe sadaka kama Musa alivyoamuru, kuwa ushuhuda kwa watu wote kwamba umetakaswa.”


“Angalisho, usimwambie mutu hata neno moja juu ya hii. Lakini kwenda kwa kuhani na kumwonyesha jinsi unavyokuwa sasa. Kisha utoe sadaka kama Musa alivyoamuru, kuwa ushuhuda kwa wote kwamba umetakaswa.”


Yesu akamwamuru hivi: “Usimwambie mutu neno juu ya hii. Lakini kwenda na kumwonyesha kuhani jinsi unavyokuwa sasa. Kisha utoe sadaka kama Musa alivyoamuru, kuwa ushuhuda kwa watu wote kwamba umetakaswa.”


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Maana mukate Mungu anaoupana ni yule anayeshuka toka mbinguni na kuleta uzima katika dunia.”


Mimi ni ule mukate wa uzima, ulioshuka toka mbinguni. Kama mutu akikula mukate huu ataishi milele. Na mukate nitakaotoa ni mwili wangu, utakaotolewa kusudi dunia ipate uzima.”


Lakini mulikombolewa kwa njia ya damu yenye bei kali ya Kristo, aliyekuwa kama kondoo asiyekuwa na kilema wala uchafu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ