Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 13:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kuhani atamwangalia tena, na kama ule upele umeenea kwenye ngozi, basi, kuhani atamutangaza mutu yule kuwa muchafu, huo ni ukoma.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 13:8
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ikiwa mutu yeyote atakuwa na kivimba au upele au chunuku juu ya mwili wake, ikionekana kwamba ni ukoma, basi, ataletwa kwa kuhani Haruni au mumoja wa wana wake anayekuwa kuhani.


Kuhani atachunguza pahali panapokuwa ugonjwa na ikiwa nywele za pahali pale zimebadilika kuwa nyeupe na ugonjwa wenyewe ukionekana kuwa uko ndani zaidi ya ngozi ya mwili wake, basi, huo ni ukoma. Kuhani akimaliza kumuchunguza, hivyo atatangaza kwamba mutu yule ni muchafu.


Lakini taka lile likienea kwenye ngozi, nyuma ya mutu yule kujionyesha kwa kuhani kwa ajili ya kutakaswa kwake, basi, atakuja tena kwa kuhani.


Kama mutu ameshikwa na ukoma, ataletwa kwa kuhani.


Uwaamuru Waisraeli wamutoe inje ya kambi kila mutu mwenye ukoma, kila mutu anayetokwa usaha, na kila anayekuwa muchafu kwa kugusa maiti.


Wewe hauna sehemu wala haki yoyote katika jambo hili, kwa sababu moyo wako si mukamilifu mbele ya Mungu.


Wanawaahidi watu wengine kwamba watakuwa huru ijapokuwa wao wenyewe ni watumwa wa upotovu. Kwa maana kila mutu ni mutumwa wa jambo lolote linalomutawala.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ