Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 13:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Lakini ikiwa kipele hicho, ingawa ni cheupe hakikuingia ndani sana ya ngozi na wala nywele za pahali pale hazikubadilika kuwa nyeupe, basi, kuhani atamutenga mutu yule kwa muda wa siku saba.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 13:4
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walawi walioniacha wakati ule Waisraeli walipojitenga nami kwa kufuata miungu yao, watabeba azabu yao.


huo ni ukoma wa muda murefu. Kuhani atamutangaza mutu yule kuwa muchafu. Hatamutenga mutu yule kwa uchunguzi maana yeye ni muchafu.


kuhani atapaangalia. Kama akiona kwamba nywele zimegeuka kuwa nyeupe na pana shimo, basi, huo ni ukoma. Ukoma huo umejitokeza kwa njia ya pahali pale palipoungua. Kuhani atamutangaza mutu yule kuwa muchafu, maana ana ugonjwa wa ukoma.


Lakini kama kuhani akiona kwamba nywele za pahali pale si nyeupe na hakuna shimo lakini pamefifia, basi, kuhani atamutenga mutu yule kwa muda wa siku saba.


Kuhani atachunguza pahali panapokuwa ugonjwa na ikiwa nywele za pahali pale zimebadilika kuwa nyeupe na ugonjwa wenyewe ukionekana kuwa uko ndani zaidi ya ngozi ya mwili wake, basi, huo ni ukoma. Kuhani akimaliza kumuchunguza, hivyo atatangaza kwamba mutu yule ni muchafu.


Kama kuhani ataona kwamba hakuna shimo na nywele si nyeusi, basi kuhani atamutenga mutu yule kwa muda wa siku saba.


Siku ya saba, kuhani atamwangalia tena mutu yule, na ikiwa, kulingana na uchunguzi wa kuhani, ugonjwa huo haujaenea kwenye ngozi yake, basi, kuhani atamutenga mutu yule kwa siku zingine saba.


Kuhani ataangalia taka lile na kuweka nguo ile kando kwa muda wa siku saba.


basi, kuhani atatoka inje kwenye mulango na kufunga nyumba hiyo kwa muda wa siku saba.


Lakini Yawe akamwambia Musa: Kama baba yake angemutemea mate kwenye uso, basi, hangepata haya kwa siku saba? Basi, umutoe inje ya kambi akae kule muda wa siku saba, kisha unaweza kumuruhusu arudi katika kambi.


Kwa hiyo, Miriamu akafukuzwa inje ya kambi kwa muda wa siku saba. Watu hawakuanza tena safari mpaka Miriamu aliporudishwa tena katika kambi.


Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.


kwamba watu fulani wa ovyo ovyo kati yenu, wamewashawishi watu wa muji wakisema: ‘Twende tuabudu miungu mingine’, ambayo bado hamukujua,


Zambi za watu wamoja zinaonekana waziwazi hata mbele hawajahukumiwa. Lakini zambi za wengine zinajulikana kisha.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ