kuhani ataangalia ugonjwa huo. Ikiwa kuhani ataona kwamba kuna shimo na nywele ni manjano na nyembamba, basi, atamutangaza mutu yule kuwa muchafu, maana huo ni upele na ni ukoma wa kichwa au wa kidevu.
Lakini ikiwa kuhani ataona kwamba vile vipele vimepona na nywele nyeusi zimeota pahali pale, basi, vidonda vimepona, basi, mutu yule ni safi. Kuhani atamutangaza mutu yule kuwa safi.