Basi, kisha kushauriana na wengine, akatengeneza sanamu mbili za zahabu. Kisha akawaambia watu: “Enyi watu wa Israeli, hii ndiyo miungu yenu iliyowatoa katika inchi ya Misri! Hakuna sababu ya kwenda Yerusalema kutoa sadaka kule.”
tafazali, chochote ambacho mutu yeyote au watu wako wote wa Waisraeli wanakuomba na kukusihi, kila mutu akijua taabu ndani ya moyo wake na kunyoosha mikono yake kuelekea nyumba hii,
tafazali usikilize maombi yoyote yatakayoombwa na mutu yeyote au watu wako wote Waisraeli, kila mutu akijua taabu yake na huzuni yake akikuomba naye akinyoosha mikono yake kuelekea nyumba hii,
Yawe aliniambia hivi: Wewe mwanadamu, utwae upanga mukali, uutumie kama wembe wa kinyozi. Unyoe kichwa na ndevu zako. Kisha utwae mizani, upime nywele zako na kuzigawanya kwa sehemu mbalimbali.
Lakini, kama ile alama haijaenea, lakini imefifia, hicho ni kivimba kilichotokana na kuungua. Basi, kuhani atamutangaza mutu yule kuwa safi, maana hilo ni kovu la kuungua.
kuhani ataangalia ugonjwa huo. Ikiwa kuhani ataona kwamba kuna shimo na nywele ni manjano na nyembamba, basi, atamutangaza mutu yule kuwa muchafu, maana huo ni upele na ni ukoma wa kichwa au wa kidevu.
Waamuzi wanahukumu kwa kupewa kutuliro, makuhani wake wanafundisha kwa kupata malipo, manabii wanatabiri kwa kupata feza. Hata hivyo wanajidai kumutegemea Yawe, wakisema: Yawe, si yupo pamoja nasi? Hatutapatwa na hasara yoyote!
Lakini kama macho yako yanaharibika, mwili wako wote utabaki katika giza. Basi ikiwa mwangaza unaokuwa ndani yako umegeuka kuwa giza, giza hilo ni nzito sana!