Ikiwa mutu yeyote atakuwa na kivimba au upele au chunuku juu ya mwili wake, ikionekana kwamba ni ukoma, basi, ataletwa kwa kuhani Haruni au mumoja wa wana wake anayekuwa kuhani.
Lakini kama kuhani akiona kwamba nywele za pahali pale si nyeupe na hakuna shimo lakini pamefifia, basi, kuhani atamutenga mutu yule kwa muda wa siku saba.
Lakini, kama ile alama haijaenea, lakini imefifia, hicho ni kivimba kilichotokana na kuungua. Basi, kuhani atamutangaza mutu yule kuwa safi, maana hilo ni kovu la kuungua.