Yuda akavitambua vitu hivyo, akasema: “Tamari ni mwenye haki kuliko mimi. Ni kweli, maana sikumwoesha kwa mwana wangu Sela.” Tokea siku hiyo Yuda hakulala tena na Tamari.
Lakini kama kuhani akiona kwamba nywele za pahali pale si nyeupe na hakuna shimo lakini pamefifia, basi, kuhani atamutenga mutu yule kwa muda wa siku saba.
naye Petro akakumbuka maneno yale Yesu aliyomwambia kwamba mbele jogoo hajawika, atakuwa amemukana mara tatu. Basi akatoka inje, akalia kwa uchungu sana.
Wandugu zangu, kama mutu akipatikana na kosa fulani, ninyi munaoongozwa na Roho wa Mungu mumwonye mutu yule kwa roho ya upole. Na kila mumoja wenu ajiangalie mwenyewe, kusudi asijaribiwe vilevile.