Kama hawezi kutoa mwana-kondoo, basi, ataleta hua wawili au vitoto viwili vya njiwa; mumoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya zambi. Kuhani atamufanyia mama huyo ibada ya upatanisho, naye atakuwa safi.
Ikiwa mutu yeyote atakuwa na kivimba au upele au chunuku juu ya mwili wake, ikionekana kwamba ni ukoma, basi, ataletwa kwa kuhani Haruni au mumoja wa wana wake anayekuwa kuhani.
Yesu alipokuwa katika muji mumoja kati ya miji ile, kukatokea mutu aliyejaa na ukoma mwili wote. Naye alipomwona Yesu, akainama uso mpaka chini, akamusihi akisema: “Bwana, kama ukitaka, unaweza kunitakasa.”