Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 12:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Siku za kutakaswa kwake zitakapotimia, ikuwe amepata mutoto mwanaume au mwanamuke, atamuletea kuhani kwenye mulango wa hema la mukutano mwana-kondoo wa mwaka mumoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na kitoto cha njiwa au hua, kwa ajili ya sadaka ya zambi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 12:6
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akamwambia: “Uniletee ngombe dike wa miaka mitatu, mwana-mbuzi dike wa miaka mitatu, kondoo dume wa miaka mitatu, na hua na kitoto cha njiwa.”


Uwaambie watu wa Israeli hivi: Mwanamuke akipata mimba na kuzaa mutoto mwanaume, atakuwa muchafu kwa muda wa siku saba sawa vile anavyokuwa kwa wakati wake wa ugonjwa wa mwezi.


Lakini, kama amezaa mutoto mwanamuke, basi, atakuwa muchafu kwa muda wa majuma mawili kama vile inavyokuwa kwa wakati wa ugonjwa wake wa mwezi. Ataendelea katika kutakasika kwake kwa muda wa siku makumi sita na sita.


Kuhani atamutolea mbele ya Yawe na kumufanyia huyo mama ibada ya upatanisho mbele ya Yawe. Hivyo huyo mwanamuke atakuwa safi kwa ajili ya kutokwa na damu yake. Hii ni sheria inayoelekea mwanamuke yeyote anayezaa mutoto mwanaume au mwanamuke.


Ataleta vilevile hua wawili au vitoto viwili vya njiwa kadiri anavyoweza mumoja atakuwa kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.


Siku ya nane, anapaswa kuleta hua wawili au vitoto viwili vya njiwa mbele ya Yawe kwenye mulango wa hema la mukutano na kumupatia kuhani.


Siku ya nane atatwaa hua wawili au vitoto viwili vya njiwa na kumuletea kuhani kwenye mulango wa hema la mukutano.


Katika siku ya nane atapeleka hua wawili au vitoto viwili vya njiwa kwa kuhani kwenye mulango wa hema la mukutano.


Siku zilipotimia za Maria na Yosefu kutakaswa kama vile Sheria ya Musa inavyoagiza, wakamupeleka mutoto Yerusalema, kusudi wapate kumutolea kwa Bwana.


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ