Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 11:45 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

45 Kwa sababu ni mimi Yawe niliyewatoa katika inchi ya Misri kusudi nikuwe Mungu wenu; kwa hiyo mukuwe watakatifu kwa maana mimi ni mutakatifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 11:45
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Nitasimamisha agano langu nawe, wazao wako na vizazi vyao vyote milele; nitakuwa Mungu wako na Mungu wa wazao wako milele.


Yawe akamwambia Musa: “Kwenda kwa watu uwatakase leo na kesho. Uwaambie wafue nguo zao


Mutakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’ Hayo ndiyo maneno utakayowaambia Waisraeli.”


Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.


Ninyi mutakuwa watu waliotakaswa kwa ajili yangu. Kwa hiyo hamutakula nyama ya nyama aliyeuawa na nyama wa pori. Nyama hiyo mutaitupia imbwa.


Nitawafanya kuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu. Ninyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika nira za Wamisri.


Israeli alipokuwa mutoto, nilimupenda. Kutoka Misri nilimwita mwana wangu.


Kwa sababu mimi ni Yawe, Mungu wenu, mujitakase na kuwa watakatifu kwa maana mimi ni mutakatifu. Wala musijichafue na kitu chochote kinachotambaa juu ya inchi.


Hiyo basi, ndiyo sheria kuelekea nyama, ndege na viumbe vyote vyenye uzima ambavyo vinaishi ndani ya maji na inchi kavu,


Uwaambie Waisraeli wote pamoja hivi: Mukuwe watakatifu maana mimi Yawe, Mungu wenu, ni mutakatifu.


Munapaswa kutumia mizani ya kweli na vipimo vinavyokuwa vya kweli. Mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri.


Kwa hiyo, mujitakase mukuwe watakatifu, maana mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Ni mimi niliyewatoa katika inchi ya Misri kusudi nikuwe Mungu wenu. Mimi ni Yawe.


Mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyekutoa kutoka inchi ya Misri kwa kukupa inchi ya Kanana, na kusudi nami nikuwe Mungu wako.


Hapana! Kwa ajili yao nitakumbuka agano nililofanya na wazee wao ambao niliwatoa katika inchi ya Misri, mataifa yakishuhudia, kusudi mimi nikuwe Mungu wao. Mimi ni Yawe.


Vishada hivyo vitawakumbusha amri zangu zote na mutazifuata zote kwa ukamilifu, nanyi mutakuwa watakatifu wangu.


Kwa maana Mungu hakutuita kusudi tuishi katika uchafu, lakini katika utakatifu.


Lakini Yoshua akawaambia: “Ninyi hamuwezi kumutumikia Yawe, maana yeye ni Mungu Mutakatifu. Yeye ni Mungu mwenye wivu, naye hatawasamehe makosa na zambi zenu.


Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Muwe watakatifu, kwa maana mimi ni mutakatifu.”


Hakuna anayekuwa mutakatifu kama Yawe; hakuna yeyote anayekuwa kama yeye; hakuna anayekuwa jiwe la kufichamia kama Mungu wetu.


Kisha, wakaaji wa muji wa Beti-Semesi wakasema: “Nani anayeweza kusimama mbele ya Yawe, huyu Mungu mutakatifu? Atakwenda kwa nani kusudi aondoke kwetu?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ