37 Ikiwa sehemu ya muzoga inaangukia mbegu za kupanda, mbegu hizo hazitakuwa chafu.
Hata hivyo, kisima au chemichemi ya maji vitakuwa safi. Lakini kitu chochote kinachogusa muzoga kitakuwa kichafu.
Lakini ikiwa mbegu zimetiwa katika maji kwa kuota na sehemu yoyote ya muzoga ikaziangukia, basi, mbegu hizo ni chafu kwenu.
Kile unachopanda si mumea muzima utakaopaswa kutokea nyuma, lakini ni punje tu, labda ya ngano au mbegu ingine fulani.
Kwa maana mumezaliwa upya, kwa nguvu za neno la Mungu lenye uzima na linalodumu hata milele. Nanyi si kama watoto waliozaliwa na wazazi wenye mwili huu unaokuwa wa kufa, lakini watoto waliozaliwa kwa nguvu ya uzazi usioweza kufa.
Kila mutu anayekuwa mutoto wa Mungu hafanyi zambi, kwa sababu neno la Mungu linakaa ndani yake; tena hawezi kufanya zambi, maana Mungu ni baba yake.
Tunajua kwamba kila mutoto wa Mungu hafanyi zambi, kwa maana Mwana wa Mungu anamulinda, wala yule Mwovu hawezi kumugusa.