Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 11:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Kugusa nyama fulanifulani kunamufanya mutu kuwa muchafu. Yeyote atakayegusa mizoga yao atakuwa muchafu mpaka magaribi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 11:24
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe wa majeshi alinifunulia haya akisema: Hakika uovu huu hautasahauliwa mbele ya kufa kwenu. Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Lakini wadudu wengine wote wenye mabawa na miguu mine ni wachafu kwenu.


Mutu akitwaa sehemu ya mizoga yake atakuwa muchafu mpaka magaribi na nguo zake zinapaswa kufuliwa.


Hao wote ni wachafu kwenu na yeyote atakayegusa mizoga yao, atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Kwa sababu nyama hao ni wachafu, musikule nyama yao wala musiguse mizoga yao.


Zaidi ya hayo, yeyote atakayeingia ndani ya nyumba hiyo wakati itakapokuwa imefungwa, atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote atakayegusa kitu chochote mutu huyu alichoikalia atakuwa muchafu mpaka magaribi. Mutu yeyote anayebeba kitu chochote kilichokuwa cha mutu huyu anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote anayetokwa na usaha akimugusa mutu bila kusafisha kwanza mikono yake na kuoga, aliyeguswa atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Kuhani atatoa hao, mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kuhani atamufanyia mutu huyu ibada ya upatanisho mbele ya Yawe na kumwondolea uchafu wake wa kutokwa na usaha.


Mutu yeyote atakayegusa kitanda cha huyo mwanamuke anapaswa kufua nguo zake na kuoga kwa maji. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote atakayegusa kitu chochote mwanamuke huyo anachoikalia anapaswa kufua nguo zake na kuoga kwa maji, naye atakuwa muchafu mupaka magaribi.


Mwanaume yeyote atakayegusa kitu chochote mwanamuke yule alicholalia au kuikalia, atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote atakayegusa vitu hivyo, atakuwa muchafu na anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote atakayegusa kitanda cha mutu yule anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote atakayeikalia kitu chochote mutu huyu mwenye kutokwa na usaha alichoikalia, anapaswa kufua nguo na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote atakayegusa mutu anayetokwa na usaha, anapaswa kufua nguo zake na kuoga; naye atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote akitemewa mate na mutu anayetokwa usaha, yule aliyetemewa mate anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Yule mutu aliyepeleka yule beberu kwa Azazeli kwanza atafua nguo zake na kuoga ndipo atakapoweza kuingia ndani ya kambi.


Yule mutu atakayewateketeza atafua nguo zake na kuoga, ndipo atakapoweza kuingia katika kambi.


Mutu yeyote wa kizazi cha Haruni akiwa na ugonjwa wa ukoma au anatokwa usaha asikule vitu vitakatifu mpaka atakapokuwa safi. Mutu yeyote akigusa mutu aliyejichafua kwa kugusa maiti au mutu aliyetokwa na mbegu za uzazi,


au akigusa kiumbe chochote chenye kutambaa ambacho kinamufanya mutu kuwa muchafu au mutu ambaye anaweza kumuchafua wa aina yoyote,


mutu huyu, atakuwa muchafu mpaka magaribi na haruhusiwi kula vyakula vitakatifu mpaka pale atakapokuwa ameoga.


Au kama mutu yeyote kati yenu akijichafua bila kukusudia kwa kugusa kitu chochote kichafu, ikuwe ni muzoga wa nyama wa pori au wa kufugwa au wadudu, atakuwa na kosa.


Mutu yeyote anayegusa kitu chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu, au kitu cha mutu kinachohesabiwa kuwa kichafu, au nyama anayehesabiwa kuwa muchafu, au kitu chochote kinahesabiwa kuwa kichafu ambacho ni chukizo, akikula nyama ya sadaka ya amani Yawe aliyotolewa, mutu huyo atatengwa na watu wake.


Nyuma ya hayo, kuhani atafua nguo zake na kuoga mwili kwa maji, halafu anaweza kuingia katika kambi; atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Musidanganyike: “Warafiki wabaya wanaharibu tabia nzuri za watu.”


Kwa sababu hiyo Bwana anasema: “Mutoke kati yao, mujitenge nao. Musiguse kitu chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu, nami nitawapokea.


Musishiriki katika matendo ya giza yasiyofaa, lakini muyafichue.


Ninyi mumekufa pamoja na Kristo na kukombolewa toka katika uwezo wa roho mbaya zinazotawala dunia. Kwa nini munaishi tena kama watu wa dunia mukilazimishwa kushika kanuni kama hizi:


Ingekuwa hivi, ingemupasa ateswe mara nyingi tangu kuumbwa kwa dunia. Lakini sasa, wakati ukikaribia kwa mwisho, yeye alitokea mara moja tu kusudi awasamehe watu zambi kwa njia ya kujitoa mwenyewe sadaka.


Lakini kama tunaishi katika mwangaza kama vile Mungu mwenyewe anavyokaa katika mwangaza, tunashirikiana sisi kwa sisi, na damu ya Mwana wake Yesu inasafisha zambi zetu zote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ