Mutu yeyote atakayegusa kitu chochote mutu huyu alichoikalia atakuwa muchafu mpaka magaribi. Mutu yeyote anayebeba kitu chochote kilichokuwa cha mutu huyu anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.
Kuhani atatoa hao, mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kuhani atamufanyia mutu huyu ibada ya upatanisho mbele ya Yawe na kumwondolea uchafu wake wa kutokwa na usaha.
Mutu yeyote wa kizazi cha Haruni akiwa na ugonjwa wa ukoma au anatokwa usaha asikule vitu vitakatifu mpaka atakapokuwa safi. Mutu yeyote akigusa mutu aliyejichafua kwa kugusa maiti au mutu aliyetokwa na mbegu za uzazi,
Au kama mutu yeyote kati yenu akijichafua bila kukusudia kwa kugusa kitu chochote kichafu, ikuwe ni muzoga wa nyama wa pori au wa kufugwa au wadudu, atakuwa na kosa.
Mutu yeyote anayegusa kitu chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu, au kitu cha mutu kinachohesabiwa kuwa kichafu, au nyama anayehesabiwa kuwa muchafu, au kitu chochote kinahesabiwa kuwa kichafu ambacho ni chukizo, akikula nyama ya sadaka ya amani Yawe aliyotolewa, mutu huyo atatengwa na watu wake.
Ninyi mumekufa pamoja na Kristo na kukombolewa toka katika uwezo wa roho mbaya zinazotawala dunia. Kwa nini munaishi tena kama watu wa dunia mukilazimishwa kushika kanuni kama hizi:
Ingekuwa hivi, ingemupasa ateswe mara nyingi tangu kuumbwa kwa dunia. Lakini sasa, wakati ukikaribia kwa mwisho, yeye alitokea mara moja tu kusudi awasamehe watu zambi kwa njia ya kujitoa mwenyewe sadaka.
Lakini kama tunaishi katika mwangaza kama vile Mungu mwenyewe anavyokaa katika mwangaza, tunashirikiana sisi kwa sisi, na damu ya Mwana wake Yesu inasafisha zambi zetu zote.