Musitoke inje ya mulango wa hema la mukutano, kama sivyo mutakufa. Maana mafuta ya kupakaa ya Yawe yangali juu yenu. Haruni na wana wake wakafanya kama vile Musa alivyosema.
Munapoingia ndani ya hema la mukutano, wewe na wana wako musikunywe divai wala kileo chochote, kama sivyo mutakufa. Hili litakuwa sharti ambalo vizazi vyenu vyote wanapaswa kulifuata siku zote.