Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 10:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Kisha Musa akamwambia Haruni na wana wake, Eleazari na Itamari: Musivuruge nywele zenu wala musipasue nguo zenu kwa kuomboleza, kama sivyo mutakufa na kuwaletea Waisraeli wote pamoja kasirani ya Yawe. Lakini wandugu zenu, ni kusema jamii yote ya Israeli, wanaweza kuomboleza kwa sababu ya moto huo Yawe alioleta.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 10:6
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa mara nyingine, Yawe aliwakasirikia Waisraeli, akamusukuma Daudi kuwatendea vibaya, akamwambia awahesabu watu wa Israeli na watu wa Yuda.


mwana wa Abisua mwana wa Finehasi mwana wa Eleazari mwana wa Haruni, Kuhani Mukubwa.


Walifanya hivyo maana Yawe alikuwa amemwambia Musa: Uwaambie Waisraeli: Ninyi ni watu wenye vichwa vigumu. Nikienda pamoja nanyi kwa muda mufupi tu, nitawaangamiza. Hivyo muvue mapambo yenu kusudi nijue namna ya kuwatendea.


Haruni alimwoa Eliseba, binti ya Aminadabu, dada ya Nasoni; naye akamuzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Itamari.


Munyoe nywele zenu na kuzitupa, enyi wakaaji wa Yerusalema: mufanye maombolezo juu ya vichwa vya milima, maana, mimi Yawe nimewakataa ninyi, nimewatupilia ninyi kizazi kilichosababisha hasira yangu!


Mwenye ukoma yeyote atavaa nguo zilizochanika, nywele zake hatazichanuliwa, na mudomo wake wa juu ataufunika na atalalamika akisema: Mimi ni muchafu, mimi ni muchafu.


Enyi watu wa Yuda, munyoe vichwa vyenu kwa kuwaomboleza watoto wenu wapenzi; mupanue upaa wenu ukuwe mupana kama wa tai, maana watoto wenu watawaacha kwenda katika uhamisho.


Lakini Walawi watapiga kambi zao kuzunguka hema la kuchunga vibao vya agano kusudi walilinde na kasirani yangu isiwake juu ya Waisraeli.


Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune, ambao walikuwa kati ya wale watu waliokwenda kupeleleza hiyo inchi, wakararua nguo zao


Lakini Musa na Haruni wakajitupa uso mpaka chini na kusema: Ee Yawe unayekuwa asili ya uzima wa wanadamu wote. Mutu mumoja akikukosea, utakasirikia watu wote pamoja?


Ninyi mutafanya kazi za Pahali Patakatifu na mazabahu, kusudi kasirani yangu isiwatokee tena Waisraeli.


Umutwae Haruni na mwana wake Eleazari, uwalete juu ya mulima Hori.


Kuhani atamuweka mbele ya Yawe na kumufunua nywele na kumupa sadaka hiyo ya vyakula inayotolewa kwa sababu ya wivu wa mume wake. Kuhani mwenyewe atashikilia kile chombo chenye maji machungu yanayoleta laana.


Walawi waliacha wazazi wao, wakawasahau wandugu zao, hawakuwatambua hata watoto wao, maana walifuata amri zako, na kushika agano lako.


Kwa nini, basi, mumeacha kumufuata Yawe? Mukimwasi Yawe leo, kesho atakasirikia sana Waisraeli wote pamoja.


Akana mwana wa Zera alipokosa uaminifu katika vitu vitakatifu, kasirani haikuangukia Waisraeli wote pamoja? Tena Akana hakukufa tu yeye peke yake kwa sababu ya uovu wake.’ ”


Lakini Waisraeli hawakukuwa waaminifu juu ya vile vitu vilivyotolewa viangamizwe maana Akana mwana wa Karmi, mujukuu wa Zabedi, wa ukoo wa Zera, wa kabila la Yuda, alitwaa vimoja kati ya vitu vilivyoamriwa viteketezwe. Kwa hiyo hasira ya Yawe ikawaka juu ya Waisraeli.


Waisraeli wametenda zambi, maana wamelivunja agano langu nililowaamuru washike. Wametwaa vimoja kati ya vitu vilivyotolewa viangamizwe. Wameviiba na kudanganya, wakaviweka pamoja na vitu vyao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ