Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 10:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Basi, moto ukatokea mbele ya Yawe, ukawateketeza hao vijana, wakakufa mbele yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 10:2
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu, hasira ya Yawe ikawaka juu ya Uza. Mungu akamwua palepale. Uza akakufa palepale pembeni ya Sanduku la Mungu.


Muzee akaenda, akaikuta maiti ya mutu wa Mungu katika barabara, simba na punda wake pembeni yake. Yule simba hakuikula maiti wala hakumushambulia punda.


Mara moja, Yawe akashusha moto, ukaiteketeza sadaka ile ya kuteketezwa, kuni, mawe na mavumbi, na kuyakausha maji yote katika mufereji.


Elia akamujibu yule kiongozi wa watu makumi tano: “Kama kweli mimi ni mutu wa Mungu, moto ushuke kutoka mbinguni na kukuteketeza wewe pamoja na watu wako!” Mara moja moto ukashuka kutoka mbinguni, ukamuteketeza pamoja na watu wake makumi tano.


Elia akamujibu: “Kama kweli mimi ni mutu wa Mungu, moto ushuke kutoka mbinguni na kukuteketeza wewe pamoja na watu wako!” Mara moja moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamuteketeza pamoja na watu wake makumi tano.


Mara moja Yawe akamukasirikia Uza kwa kuligusa sanduku, akamwua. Uza akakufa palepale mbele ya Mungu.


Kwa sababu hamukulibeba safari ya kwanza, Yawe, Mungu wetu, akatuazibu maana hatukulitunza kama vile alivyoagiza.”


Nadabu na Abihu walikufa mbele ya baba yao, wala hawakukuwa na watoto; kwa hiyo wandugu zao Eleazari na Itamari wakakuwa makuhani.


Alipokuwa hajamaliza kusema, mwingine akafika, akasema: “Umeme wa radi umewachoma na kuwateketeza kondoo na watumishi. Ni mimi tu peke yangu nimepona kwa kuja kukuletea habari.”


Mungu wetu anakuja, lakini si kimyakimya: moto wenye kuteketeza unamutangulia, na zoruba kali inamuzunguka.


Yawe akamwambia Musa: Mukuje kwangu, wewe Haruni, Nadabu na Abihu, pamoja na wazee makumi saba wa Israeli, muniabudu kwa mbali.


Kweli, pahali pa kumuteketeza mufalme wa Asuria pamekwisha kutayarishwa muda murefu uliopita. Pahali penyewe ni shimo kubwa na pana. Kuna moto na kuni kwa uwingi. Yawe ataupulizia pumzi yake kama kijito cha kiberiti na kuuwasha.


Wakatwaa maiti za wandugu zao na kuzipeleka inje ya kambi wakiwa wamevaa nguo zao, kama vile Musa alivyoamuru.


Yawe akazungumuza na Musa, kisha kufa kwa wana wawili wa Haruni wakati ule walipomukaribia.


Yawe akawasha moto ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa na mafuta yaliyokuwa juu ya mazabahu. Watu wote walipoona huo moto wakapiga vigelegele na kuinama uso mpaka chini.


watu hao waliotoa habari za uongo juu ya hiyo inchi, wakakufa kwa pigo mbele ya Yawe.


Kisha Yawe akashusha moto ukawateketeza wale watu mia mbili makumi tano waliokwenda kufukiza ubani.


Nadabu na Abihu walikufa walipomutolea Yawe sadaka ya moto usiofaa.


Mara moja Safira akaanguka chini mbele ya Petro na kufa. Halafu wale vijana wakaingia ndani, wakamukuta amekwisha kufa. Basi wakamubeba mbali na muji na kumuzika kule karibu na mume wake.


Anania aliposikia maneno hayo, mara moja akaanguka chini na kufa. Na wote waliosikia habari ile wakashikwa sana na woga.


Mambo haya yote yaliwafikia kusudi yakuwe mufano kwa watu wengine; yameandikwa kwa kutuonya sisi, kwa maana tunaishi katika kipindi cha mwisho wa nyakati.


Yawe aliwaua wakaaji makumi saba wa muji wa Beti-Semesi, kwa sababu waliangalia ndani ya Sanduku lake. Watu waliomboleza kwa sababu Yawe alikuwa amefanya mauaji makubwa kati yao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ