Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 10:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Haruni akamwambia Musa: Angalia, leo wametolea sadaka yao ya kuondoa zambi na sadaka ya kuteketezwa mbele ya Yawe; hata hivyo mambo haya yamenipata! Tena kama ningekula ile sadaka kwa ajili ya zambi hivi leo, ingekubalika mbele ya Yawe?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 10:19
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe anasema hivi: Uwingi wa sadaka zenu ni kitu gani kwangu? Nimechoka na sadaka zenu za kondoo wenye kuteketezwa na mafuta ya nyama wenu wenye kunona. Sipendezwi na damu ya ngombe dume, wala ya wana-kondoo, wala ya beberu.


Munapoinua mikono yenu kwa kuomba, nitauficha uso wangu nisiwaone. Hata mukiomba sana sitawasikia, maana mikono yenu imejaa damu.


Hata wakifunga, sitayasikiliza maombi yao, na hata wakinitolea sadaka za kuteketeza kwa moto na sadaka zingine, mimi sitazikubali. Lakini nitawaangamiza kwa vita, njaa na ugonjwa mukali.


Kwa nini kuniletea ubani kutoka Seba, na udi wa harufu nzuri kutoka inchi ya mbali? Sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto hazikubaliki, wala sadaka zenu zingine hazinipendezi.


Hawatamutolea Yawe sadaka ya divai, wala hawatamufurahisha kwa sadaka zao. Chakula chao kitakuwa kama cha kilio, wote watakaokikula watajichafua. Kitakuwa chakula cha kuwashibisha tu, hakitafaa kuletwa katika nyumba kwa Yawe.


Kisha Haruni akamuchinja nyama wa sadaka ya kuteketezwa. Wana wake wakamuletea damu, naye akainyunyizia mazabahu pande zote.


Basi, Haruni akakaribia mazabahu, akachinja yule mwana-ngombe aliyemutoa kuwa sadaka kwa ajili ya zambi yake mwenyewe.


Heri kungepatikana mutu mumoja kati yenu ambaye angefunga milango ya hekalu kusudi musiwashe moto usiokubaliwa kwenye mazabahu yangu! Sipendezwi nanyi na sitaikubali sadaka yoyote munayonitolea.


Munasema: Mambo haya yametuchokesha sana na munanizarau. Munaniletea sadaka za nyama muliopata kwa njia ya kunyanganya, au wanaokua vilema au wagonjwa. Basi, nipokee sadaka hizo toka katika mikono yenu?


Zaidi ya hayo yote, munaifunika mazabahu ya Yawe kwa machozi yenu, mukilia na kuomboleza kwa sababu yeye hazikubali tena sadaka munazomutolea.


Huko, mutakula mbele ya Yawe, Mungu wenu, na mutafurahi ninyi pamoja na watu wa nyumba zenu kwa ajili ya mafanikio yenu Yawe, Mungu wenu, aliyowabarikia.


Sikukula sehemu ya kumi yoyote nilipokuwa ninaomboleza; sikuitoa inje ya nyumba yangu nilipokuwa muchafu na sikutoa sehemu ya kumi hiyo kwa wafu. Nimekutii ee Yawe, Mungu wangu; nimefanya kila kitu ulichoamuru juu ya sehemu ya kumi.


Mufurahi siku zote katika kuungana kwenu na Bwana. Na tena ninasema: Mufurahi!


Yeye hahitaji kutoa sadaka kila siku kama vile Makuhani wengine Wakubwa, kwanza kwa ajili ya zambi zake mwenyewe na kisha kwa ajili ya zambi za watu. Kwa maana amefanya vile mara moja tu wakati alipojitoa mwenyewe kufa.


Hivi Roho Mutakatifu alikuwa akionyesha kwamba njia ya kuingia katika Pahali Patakatifu Sana ilikuwa bado kufunguliwa kwa wakati wote ile Hema ya kwanza ilipokuwa ingali ikisimikwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ