Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 10:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Lakini kilali ambacho wanafanya nacho kitambulisho cha kumutolea Yawe na muguu unaotolewa sadaka kama vile kitambulisho, munaweza kuvikulia pahali popote pasipo kuwa pachafu. Utakula wewe na watoto wako wanaume na wanawake. Vitu hivyo umepewa kama haki yako na ya wazao wako kutoka sadaka za amani za watu wa Israeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 10:14
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watakula vitu hivyo vilivyotumika kwa utakaso na kwa ajili ya kuwafanyia upatanisho, lakini mutu mwingine asiruhusiwe kuvikula maana ni vitakatifu.


Yule mutu akaniambia: Vyumba hivi vyote ni vitakatifu. Ndani ya vyumba hivi makuhani wanaoingia mbele ya Yawe, wanakula sadaka takatifu kabisa: sadaka takatifu kabisa na humo ndimo munamowekwa sadaka za vyakula, sadaka za kuomba kusamehewa zambi na sadaka kwa ajili ya malipo ya kosa kwa sababu pahali hapo ni patakatifu.


Mutaikula katika Pahali Patakatifu kwa sababu hiyo ni haki yako na wazao wako kutoka katika sadaka Yawe anazotolewa kwa moto. Hivi ndivyo nilivyoamuriwa.


Lakini kama binti ya kuhani ni mujane au amefukuzwa na mume wake na hana mutoto, naye amerudi kwa baba yake na kukaa naye kama vile alipokuwa kijana, basi, anaweza kula chakula cha baba yake. Hata hivyo, mugeni haruhusiwi kula chakula hicho.


Lakini vile vilali na ule muguu wa nyuma wa kuume, Haruni akafanya navyo kitambulisho cha kumutolea Yawe, kama vile Musa alivyoamuru.


Vilevile, vitu vingine vyote Waisraeli watakavyonitolea kama vile sadaka za kutikiswa, vitakuwa vyako. Ninakupa wewe, wana wako na wabinti zako kuwa haki yenu milele. Mutu yeyote katika jamaa yako asiyekuwa muchafu anaweza kula vitu hivyo.


Kila sadaka ya matoleo yote matakatifu ya Waisraeli watakayomuletea kuhani, itakuwa yake.


Yesu akawaambia: “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya yule aliyenituma na kutimiza kazi yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ