Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 10:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Mutawafundisha Waisraeli masharti yote ambayo nimewaambia kwa njia ya Musa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 10:11
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa muda murefu sasa, Waisraeli wameishi bila Mungu wa kweli, wala makuhani wa kuwafundisha, na bila Sheria.


Walitwaa kitabu cha Sheria ya Yawe, wakazunguka nacho katika miji yote ya Yuda wakifundisha watu.


Mufalme Hezekia aliwasifu na kuwatia moyo makuhani kwa sababu waliendesha ibada kwa ujuzi mwingi. Nyuma ya kumaliza siku saba ambamo watu walikula, wakatoa sadaka za amani na kumutukuza Yawe, Mungu wa babu zao,


Ezra, ambaye alikuwa kuhani, akaenda na kuleta kitabu cha Sheria ya Musa mbele ya mukutano wote, wanaume na wanawake na yeyote aliyeweza kuelewa ile sheria. Siku hiyo ilikuwa ni siku ya kwanza ya mwezi wa saba.


Wakasoma vizuri toka kitabu cha Sheria ya Mungu na kuifafanua na watu wote waliweza kuielewa.


Kisha, watu wakasema: Tuende tufanye shauri baya juu ya Yeremia, maana hatukosi makuhani wa kutufundisha. Vilevile hatukosi watu wenye hekima wa kutushauria na manabii wa kututangazia ujumbe wa Mungu! Mukuje tumushitaki kufuatana na maneno yake mwenyewe, wala tusiyatilie maana mambo yote anayosema.


Nao makuhani hawakujiuliza hivi: Yuko wapi Yawe? Wafundi wa sheria hawakunijua, viongozi wa watu waliniasi; manabii nao walitabiri kwa jina la Bali na kuabudu sanamu zisizokuwa na faida yoyote.


Ni kazi ya makuhani kuwafundisha watu maarifa ya kweli juu ya Mungu kusudi watu wawaendee kwa kujifunza mapenzi yangu kwao, maana makuhani ni wajumbe wa Yawe wa majeshi.


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


Ni vile kwa sababu niliwatangazia mupango wote wa Mungu pasipo kuwaficha kitu.


Kisha mutafanya kama vile watakavyowatangazia pale pahali Yawe atakapochagua. Mutakuwa waangalifu kufanya yote kama vile watakavyowaagiza.


Itawapasa kufanya kufuatana na maongozi watakayowapatia na uamuzi watakaotoa kwenu. Musiache kutimiza hukumu watakayowatangazia kwa kupita kuume au kushoto.


“Kama mutu akishikwa na ukoma munapaswa kuwa waangalifu kufuata maagizo ya Walawi. Kama vile nilivyowaamuru ndivyo mutakavyofuata kwa uangalifu.


Na watafundisha wazao wa Yakobo maagizo yako; watafundisha watu wa Israeli sheria yako. Walawi watafukiza ubani mbele yako, sadaka nzima za kuteketezwa juu ya mazabahu yako.


Kwa maana munajua maagizo gani tuliyowatolea kutoka kwa Bwana Yesu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ