Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 10:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Munapaswa kuweka tofauti kati ya mambo matakatifu na mambo yasiyokuwa matakatifu, kati ya mambo machafu na yasiyokuwa machafu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 10:10
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yawe akasema hivi: Kama ukinirudilia, nitakurudisha katika hali yako ya mbele, nawe utanitumikia tena. Kama ukisema maneno ya maana, yasiyokuwa ya upuuzi, basi utakuwa musemaji wangu. Watu watakufikia wewe, wala si wewe utakayehitaji kuwaendea.


Makuhani wao wanavunja sheria zangu, na kukufuru vyombo vyangu vitakatifu. Hawapambanui kati ya vitu vitakatifu na vitu visivyokuwa vitakatifu, wala hawafundishi watu tofauti kati ya mambo yanayokuwa machafu na yanayokuwa safi. Wameacha kuzishika Sabato zangu, na kunizaraulisha kati yao.


Makuhani watafundisha taifa langu kupambanua vitu vinavyokuwa vitakatifu na visivyokuwa vitakatifu, na kuwajulisha tofauti kati ya vitu vinavyokuwa vichafu na visivyokuwa vichafu.


kwa kutia tofauti kati ya kisichokuwa kichafu na kinachokuwa kichafu, kinachoweza kukuliwa na kisichoweza kukuliwa.


Kuhani atamwangalia. Ikiwa kuhani ataona kwamba hicho kivimba ni chekundu-cheupe kwenye upaa au kwenye paji lake na unaonekana kama ukoma kwenye ngozi yake,


kwa kuonyesha ni kitu gani kinachokuwa kichafu na kisichokuwa kichafu. Hiyo ndiyo sheria juu ya taka la ukoma.


Kila kitu ni safi kwa watu wanaokuwa safi. Lakini hakuna chochote kinachokuwa safi kwa watu wachafu na wasiomwamini Mungu, kwa maana akili na zamiri zao zimekuwa chafu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ