Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 1:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Lakini matumbotumbo na miguu ya nyama yule vitasafishwa kwa maji. Kuhani atateketeza sadaka yote juu ya mazabahu. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 1:9
35 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Harufu nzuri ya sadaka hiyo ikamupendeza Yawe, naye akasema ndani ya moyo wake: “Sitailaani tena inchi hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu. Ninajua kwamba mawazo yake ni maovu tangu utoto wake. Wala sitaangamiza tena viumbe vyote kama vile nilivyofanya.


Haruni na wazao wake ndio waliokuwa wakitoa sadaka juu ya mazabahu ya sadaka za kuteketezwa kwa moto na vilevile juu ya mazabahu ya kufukizia ubani. Walifanya kazi zote zilizoelekea Pahali Patakatifu Sana kwa kuifanyia Israeli upatanisho. Haya yote waliyafanya kulingana na maagizo Musa, mutumishi wa Mungu aliyotoa.


Akatengeneza vilevile beseni kumi za kusafishia sehemu za nyama zilizotumika katika sadaka za kuteketezwa kwa moto. Tano kati ya bakuli zile akaziweka upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Birika lilitumiwa na makuhani kwa kunawia.


Nimekukosea wewe peke yako, nimetenda mabaya mbele yako. Hivi uamuzi wako ni wa haki, hukumu yako haipotoki.


Nitakutolea sadaka za kuteketezwa za nyama wenye kunona, sadaka za kuteketezwa za kondoo dume; nitatoa sadaka za ngombe dume na beberu.


Imekatazwa kuikula ikiwa mbichi au imetokoteshwa kwa maji, lakini inapaswa kuchomwa yote, pamoja na kichwa, miguu na nyama zake za ndani.


Kisha utamuteketeza kondoo muzima juu ya mazabahu kwa kunitolea sadaka ya kuteketezwa. Harufu ya sadaka inayotolewa kwa moto itanipendeza mimi Yawe.


Kisha utavitwaa tena kutoka mikono yao na kuviteketeza juu ya mazabahu pamoja na ile sadaka ya kuteketezwa, vikuwe harufu nzuri itakayonipendeza mimi Yawe. Hiyo ni sadaka inayotolewa kwa moto.


Wewe Yerusalema, usafishe maovu ya moyo wako, kusudi upate kuokolewa. Mpaka wakati gani utaendelea kuchunga maovu?


Maana nilipowapeleka katika ile inchi niliyoapa kuwapa, kila mara walipoona kilima kirefu au miti ya majani mengi, walianza kutoa matambiko na sadaka zao na kunichokoza. Kulekule walitoa sadaka za harufu nzuri na kutoa sadaka za kinywaji.


Kisha kuwatoa toka katika inchi ambako mumesambazwa na kuwakusanya pamoja, nitazipokea sadaka zenu zenye harufu nzuri. Nami nitaonyesha utakatifu wangu kati yenu mbele ya mataifa mengine.


Kwenye kiwanja cha inje, kulikuwa chumba cha zaidi kilichounganishwa na njia ya kuingilia ya ndani kwa upande wa kaskazini. Chumba hicho kilikuwa kinaelekea baraza ya kuingilia, na huko walisafishia nyama waliochinjwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa nzima.


Lakini matumbotumbo na miguu yake atavisafisha kwa maji. Kuhani ataiteketeza yote juu ya mazabahu. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.


Atamushika mabawa na kumupasua, lakini asimwachanishe vipande viwili. Kisha, kuhani atamuteketeza kwenye mazabahu, juu ya kuni. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.


Kuhani atateketeza sehemu ya sadaka hiyo ya ngano iliyopondwa na mafuta pamoja na ubani wake wote, ikuwe sadaka ya ukumbusho. Hiyo ni sadaka Yawe anayotolewa kwa moto.


Kisha, atawaletea hao makuhani, wazao wa Haruni. Atatwaa mukono mumoja wa unga huo laini wenye mafuta na ubani na kumupelekea kuhani mumoja ambaye atauteketeza juu ya mazabahu ukuwe sadaka ya ukumbusho kwa Yawe. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.


Kuhani atatwaa sehemu ya sadaka hiyo ikiwa ni sadaka ya ukumbusho na kuiteketeza juu ya mazabahu. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.


Kuhani ataviteketeza hivyo vyote juu ya mazabahu kama vile chakula Yawe anachotolewa kwa moto.


Wazao wa Haruni wataiteketeza juu ya mazabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa inayokuwa juu ya kuni. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.


Mafuta yote ya mbuzi huyo atayaondoa kama vile anavyoondoa mafuta ya nyama wa sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya mazabahu, na harufu yake nzuri itamupendeza Yawe. Basi, kuhani atamufanyia yule mutu hiyo ibada ya upatanisho, naye atasamehewa.


Unga huo utachanganywa na mafuta na kupikwa juu ya kikaango. Kisha utauleta ukiwa vipandevipande na kumutolea Yawe na harufu ya sadaka yake itamupendeza Mungu.


Kisha kusafisha matumbotumbo na miguu kwa maji, Musa akaviteketeza vyote juu ya mazabahu pamoja na sehemu zingine za huyo kondoo kama sadaka ya kuteketezwa. Hiyo ni sadaka inayotolewa kwa moto, yenye harufu ya kumupendeza Yawe. Musa akafanya kama vile alivyoamuriwa na Yawe.


Kisha Musa akatwaa vitu hivyo vyote kutoka mikono yao na kuviteketeza juu mazabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa. Hii ni sadaka ya utakaso, yenye harufu ya kumupendeza Yawe, ni sadaka inayotolewa kwa moto.


Akasafisha matumbotumbo na vikanyagio na kuviteketeza pamoja na ile sadaka ya kuteketezwa kwenye mazabahu.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


mukinitolea mimi Yawe sadaka kutoka katika mifugo yenu, sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kutimiza kiapo au kutoa sadaka ya mapenzi au sadaka ya wakati wa sikukuu zenu zilizowekwa, na kufanya harufu nzuri ya kunipendeza mimi Yawe,


Kwa mwanzo wa kila mwezi, mutamutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume mumoja, wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wasiokuwa na kilema.


Sadaka ya kinywaji itakayotolewa na kila mwana-kondoo ni litre moja ya divai. Utaimimina sadaka hii ya kinywaji kikali Pahali Patakatifu.


Wakati wa magaribi utamutoa yule mwana-kondoo mwingine kwa kuteketezwa kwa moto, pamoja na sadaka zile za ngano na za kinywaji. Itakuwa sadaka yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.


Kwa maana sisi ni kama harufu nzuri iliyotolewa na Kristo kwa Mungu; na kunukia wale wanaookolewa na wale wanaopotea.


Muishi katika upendo kama vile Kristo alivyotupenda na kutoa maisha yake kwa ajili yetu kama vile matoleo na sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri inayomupendeza Mungu.


Hapo, mutatoa sadaka za kuteketezwa, nyama na damu, kwenye mazabahu ya Yawe, Mungu wenu. Damu ya nyama mutainyunyiza kwenye mazabahu ya Yawe Mungu wenu, lakini munaruhusiwa kula nyama.


Kweli nina vitu vyote vya lazima na zaidi kupita. Sasa kwa kuwa Epafrodito ameniletea zawadi zenu zote, ninatosheka. Zawadi hizi ni kama sadaka ya ubani yenye harufu nzuri, na kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto inayokubaliwa na Mungu na kumupendeza.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ