Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kama sadaka mutu anayotoa ni ya kuteketezwa kwa moto, atamuchagua nyama dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake, atamutolea mbele ya mulango wa hema la mukutano kusudi apate kukubaliwa na Yawe;

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 1:3
79 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Abrahamu akainua macho, akaona kondoo dume, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi, akakwenda, akamutwaa yule kondoo, akamutoa sadaka ya kuteketezwa kwa moto pahali pa mwana wake.


Mungu akamwambia: “Umutwae mwana wako, Isaka, mwana wako wa pekee unayemupenda, uende mpaka inchi ya Moria, umutoe kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto juu ya mulima nitakaokuonyesha.”


Abrahamu akamujibu: “Mwana wangu, Mungu mwenyewe atatujalia mwana-kondoo wa sadaka ya kuteketezwa.” Basi, wakaendelea na safari yao.


Noa akamujengea Yawe mazabahu, akatwaa mumoja katika kila aina ya nyama wanaohesabiwa kuwa safi na ndege anayehesabiwa kuwa safi, akamutolea Mungu sadaka za kuteketezwa kwa moto juu ya mazabahu.


Sadaka za kuteketeza walizoleta kwa jumla zilikuwa ngombe dume makumi saba, kondoo dume mia moja na wana-kondoo mia mbili. Zote hizo zilikuwa sadaka za kuteketeza kwa ajili ya Yawe.


Halafu wakatenga sadaka za kuteketeza kwa moto kusudi wapate kuzigawanya kwa watu kulingana na jamaa zao kusudi wamutolee Yawe kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Musa. Nao wakafanya vile vile na wale ngombe dume.


Watu wako watajitolea, siku utakapokwenda kuwapiga waadui. Juu ya milima mitakatifu vijana wako watakufikia, kama umande unaotokeza asubui mapema.


Halafu nikasema: “Ninakuja. Katika kitabu imeandikwa juu yangu.


Mwana-kondoo yule asikuwe na kilema chochote, akuwe dume wa mwaka mumoja. Anaweza kuwa mwana-kondoo au mwana-mbuzi.


Kisha akatuma vijana wa watu wa Israeli wamutolee Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto na kumuchinjia sadaka za amani za ngombe.


Kisha utamuteketeza kondoo muzima juu ya mazabahu kwa kunitolea sadaka ya kuteketezwa. Harufu ya sadaka inayotolewa kwa moto itanipendeza mimi Yawe.


Kisha uwapeleke Haruni na wana wake kwenye mulango wa hema la mukutano na kuwanawisha.


Sadaka hii ya kuteketezwa itatolewa siku zote, kizazi kwa kizazi, mbele yangu mimi Yawe, mbele ya mulango wa hema la mukutano ambapo mimi nitakutana nanyi na kuongea nanyi.


Kesho yake watu wakaamuka mapema wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Watu wakaikaa chini kwa kula na kunywa, kisha wakasimama na kucheza.


Kila mutu aliyevutwa na kusukumwa ndani ya moyo wake alimutolea Mungu muchango wake kwa ajili ya hema la mukutano, kazi zake zote na nguo yake takatifu.


Waisraeli wote, wanaume na wanawake, ambao walivutwa ndani ya moyo wao kuleta kitu chochote kwa ajili ya kazi ambayo Yawe alikuwa amemwagiza Musa ifanyike, walileta vitu hivyo kwa mapenzi yao, kama vile muchango wa kumupa Yawe.


Mutatoa katika mali zenu muchango wa kumupa Yawe. Kila mutu mwenye moyo mwema atamuletea Yawe muchango: sadaka, feza, shaba;


Hao wakapokea kutoka kwa Musa vitu vyote vilivyotolewa na Waisraeli kwa mapenzi yao kwa ajili ya kazi ya hema takatifu. Watu waliendelea kumuletea michango yao kufuatana na mapenzi yao kila asubui.


Akatengeneza mazabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto. Mazabahu hiyo ilikuwa ya muraba, metre mbili na sentimetre makumi mbili kwa metre mbili na sentimetre makumi mbili, na urefu kwenda juu metre moja na sentimetre makumi mbili.


Yawe anasema hivi: Uwingi wa sadaka zenu ni kitu gani kwangu? Nimechoka na sadaka zenu za kondoo wenye kuteketezwa na mafuta ya nyama wenu wenye kunona. Sipendezwi na damu ya ngombe dume, wala ya wana-kondoo, wala ya beberu.


Maana, katika mulima wangu mutakatifu, mulima murefu wa Israeli, ninyi wote watu wa Israeli mutanitumikia kule. –Ni ujumbe wa Yawe.– Huko mimi nitawapokea na kungojea muniletee sadaka na matoleo yenu bora na matoleo iliyotakaswa.


Halafu katika baraza karibu na njia kulikuwa meza mbili upande mumoja na zingine mbili upande mwingine. Meza hizo zilitumika kuwa pahali pa kuchinjia sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya usamehe wa zambi na sadaka ya malipo ya kosa.


Kama sadaka yake ya kuteketezwa ataitwaa katika kundi la kondoo au mbuzi, basi atachagua dume asiyekuwa na kilema.


Siku ya nane ataleta wana-kondoo dume wawili wasiokuwa na kilema, kondoo dike wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema, kilo tatu za unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya vyakula pamoja na mafuta sehemu moja ya tatu ya litre.


Kisha, wale beberu wawili atawaweka kwenye mulango wa hema la mukutano.


bila kumuleta nyama huyo kwenye mulango wa hema la mukutano kwa kumutolea Yawe mbele ya makao yake, mutu yule atakuwa na kosa ya kumwanga damu. Amemwanga damu na atatengwa na watu wake.


Uwaambie kwamba mutu yeyote kati ya Waisraeli au mugeni anayeishi kati yao, anayetoa sadaka ya kuteketezwa au sadaka ingine,


lakini haileti mbele ya mulango wa hema la mukutano kwa kumutolea Yawe, mutu yule atatengwa na watu wake.


Siku hiyo munapofanya kitambulisho cha kutoa huo muganda mbele yangu mutanitolea mimi Yawe sadaka ya kuteketezwa ya mwana-kondoo dume wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema.


Pamoja na hayo, mutatoa wana-kondoo saba wa mwaka mumoja, mwana-ngombe dume mumoja, na kondoo dume wawili. Nyama hao watakuwa sadaka ya kuteketezwa pamoja na sadaka ya vyakula na sadaka za kinywaji. Harufu ya sadaka hizi itanipendeza mimi Yawe.


Kama mutu anatoa sadaka ya amani na sadaka yake ni ngombe dume au dike, nyama huyo asikuwe na kilema mbele yangu.


Wazee wao wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo ngombe dume, kisha atachinjwa mbele ya Yawe.


mara tu akijulishwa zambi hiyo aliyotenda, ataleta sadaka yake ya beberu asiyekuwa na kilema.


Ikiwa kuhani ambaye amepakwa mafuta ndiye aliyetenda zambi hata akawatia watu katika kosa, basi huyo atamutolea Yawe ngombe dume muchanga asiyekuwa na kilema akuwe sadaka kwa ajili ya zambi.


Ikiwa mutu yule ataleta mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya zambi, basi, ataleta mwana-kondoo dike asiyekuwa na kilema.


Kama mutu yeyote akikosa kwa kutenda zambi bila kujua juu ya kutokutoa vitu vitakatifu Yawe anavyotolewa, atamuletea kondoo dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake. Wewe utapima bei yake kulingana na kipimo cha Pahali Patakatifu. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya kosa.


Atamuletea kuhani kondoo dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake ikiwa na bei sawa na ile ya sadaka ya kosa. Na kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa kosa alilofanya, naye atasamehewa.


Umupatie Haruni na wana wake maagizo haya: hii ndiyo sheria ya ibada juu ya sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Sadaka ya kuteketezwa itakuwa kwenye moto juu ya mazabahu usiku kucha mpaka asubui na moto wake uchochewe, usizimike.


Mumoja wa makuhani atatwaa mukono mumoja wa unga wa sadaka ya vyakula pamoja na mafuta na ubani wote na kuviteketeza juu ya mazabahu kama vile sehemu ya ukumbusho. Harufu yake itamupendeza Yawe.


Lakini kama sadaka hiyo ya amani ni ya kutimiza kiapo au ya mapenzi mema, itakuliwa siku hiyohiyo inapotolewa na sehemu ingine inaweza kukuliwa kesho yake.


Kisha, Musa akaleta kondoo dume wa sadaka ya kuteketezwa. Haruni na wana wake wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo huyo.


Kisha kusafisha matumbotumbo na miguu kwa maji, Musa akaviteketeza vyote juu ya mazabahu pamoja na sehemu zingine za huyo kondoo kama sadaka ya kuteketezwa. Hiyo ni sadaka inayotolewa kwa moto, yenye harufu ya kumupendeza Yawe. Musa akafanya kama vile alivyoamuriwa na Yawe.


Musa akamwambia Haruni: Twaa mwana-ngombe dume kwa ajili ya sadaka ya kuondoa zambi na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, nyama wote wasikuwe na kilema. Kisha uwatoe sadaka mbele ya Yawe.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


Alaaniwe mutu yeyote anayenidanganya, ambaye anaahidi kwa kiapo kunitolea sadaka ya nyama safi kutoka kundi lake, lakini ananitolea sadaka ya nyama mwenye kilema. Mimi ni mufalme mukubwa, na watu wa mataifa yote wananiogopa. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


mukinitolea mimi Yawe sadaka kutoka katika mifugo yenu, sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kutimiza kiapo au kutoa sadaka ya mapenzi au sadaka ya wakati wa sikukuu zenu zilizowekwa, na kufanya harufu nzuri ya kunipendeza mimi Yawe,


Wakati mutakapomutolea Yawe mwana-ngombe dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au sadaka kwa kutimiza kiapo au kwa ajili ya sadaka za amani,


Haya ni masharti ya sheria ambayo mimi Yawe ninatoa. Uwaambie Waisraeli wawaletee ngombe dike mwekundu mukamilifu asiyekuwa na kilema chochote, na ambaye hajapata kufungwa nira.


Mungu si mutu, hata aseme uongo, wala si mwanadamu, hata abadilishe nia yake! Ataahidi kitu na asikifanye, au kusema kitu asikitimize?


Balaki akamwambia Balamu: Kuja, nitakupeleka pahali pengine. Labda Mungu atakubali uwalaani watu hao kutoka huko kwa ajili yangu.


Halafu Balamu akamwambia Balaki: Baki hapa karibu na sadaka yako ya kuteketezwa kwa moto, nami niende. Labda Yawe atakutana nami. Chochote atakachonionyesha nitakuja kukuambia. Basi, Balamu akaenda peke yake juu ya kilele cha mulima.


Balaki akafanya kama vile alivyoambiwa na Balamu, kisha akatoa juu ya kila mazabahu ngombe dume mumoja na kondoo dume mumoja.


Kwa mwanzo wa kila mwezi, mutamutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume mumoja, wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wasiokuwa na kilema.


Mutatoa sadaka ya kuteketezwa kama vile sadaka ya ngano kwa Yawe: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume mumoja, wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wote wakuwe bila kilema.


Mutatoa vitu hivi zaidi ya ile sadaka ya kuteketezwa ya kawaida pamoja na sadaka yake ya kinywaji.


Mutatoa sadaka ya kuteketezwa kwa moto, yenye harufu nzuri inayomupendeza Yawe: wana-ngombe dume kumi na watatu, kondoo dume wawili, wana-kondoo kumi na wane wa mwaka mumoja. Wote wasikuwe na kilema.


Mutatoa sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri ya kumupendeza Yawe: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wote wakuwe wasiokuwa na kilema chochote.


Malaika akamujibu: “Roho Mutakatifu atakufikia, na uwezo wa Mungu Mukubwa utakufunika kama vile kivuli. Kwa sababu hii mutoto yule atakayezaliwa ataitwa Mutakatifu na Mwana wa Mungu.


Wakati alipomwona Yesu akipita, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu.”


Basi Yesu akaongeza kusema: “Kweli, kweli ninawaambia: mimi ni mulango wa upango wa kondoo.


Mimi ni mulango. Mutu akiingia kwa kupitia kwangu, ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata chakula.


Kwa maana kama mutu akiwa na moyo wa kutoa, Mungu anakubali kitu anachotoa kufuatana na kile anachokuwa nacho, wala si kufuatana na kile asichokuwa nacho.


Basi inafaa kila mutu atoe sawa alivyokusudia, si kwa huzuni wala si kwa kulazimishwa. Kwa maana Mungu anapenda mutu yule anayetoa kwa furaha.


Kwa maana, kwa njia ya Kristo sisi wote, Wayuda na watu wa mataifa mengine, tumefunguliwa njia ya kufika mbele ya Baba katika Roho mumoja.


Alitaka hivi kujipatia yeye mwenyewe kanisa tukufu na takatifu, lisilokuwa na taka wala kikunjo wala kilema chochote.


Hapo, mutatoa sadaka za kuteketezwa, nyama na damu, kwenye mazabahu ya Yawe, Mungu wenu. Damu ya nyama mutainyunyiza kwenye mazabahu ya Yawe Mungu wenu, lakini munaruhusiwa kula nyama.


Lakini nyama huyo akiwa na kilema chochote, ni kusema kiwete au kipofu, au ana kilema chochote kikubwa, usimutoe kuwa sadaka kwa Yawe, Mungu wako.


“Musitoe sadaka kwa Yawe, Mungu wenu, ngombe au kondoo mwenye kilema; hiyo ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu.


Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.


Ikiwa ni hivi, damu ya Kristo haitakuwa na uwezo zaidi wa kututakasa? Kwa maana kwa njia ya Roho anayeishi kwa milele, Kristo alijitoa mwenyewe kwa Mungu kuwa sadaka kamilifu. Nayo damu yake ikazitakasa zamiri zetu toka katika matendo yasiyofaa, kusudi tupate kumutumikia Mungu Mwenye Uzima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ