Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 1:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Atamushika mabawa na kumupasua, lakini asimwachanishe vipande viwili. Kisha, kuhani atamuteketeza kwenye mazabahu, juu ya kuni. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 1:17
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Abramu akamuletea hao wote, akakata kila nyama vipande viwili, akavipanga katika mistari miwili, vikielekeana. Lakini ndege hakuwakata vipande viwili.


Harufu nzuri ya sadaka hiyo ikamupendeza Yawe, naye akasema ndani ya moyo wake: “Sitailaani tena inchi hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu. Ninajua kwamba mawazo yake ni maovu tangu utoto wake. Wala sitaangamiza tena viumbe vyote kama vile nilivyofanya.


Kweli wewe unanikinga na nguvu za kuzimu, haumwachi mutakatifu wako aone kaburi.


Lakini matumbotumbo na miguu yake atavisafisha kwa maji. Kuhani ataiteketeza yote juu ya mazabahu. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.


Kisha, atawaletea hao makuhani, wazao wa Haruni. Atatwaa mukono mumoja wa unga huo laini wenye mafuta na ubani na kumupelekea kuhani mumoja ambaye atauteketeza juu ya mazabahu ukuwe sadaka ya ukumbusho kwa Yawe. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.


Wazao wa Haruni wataiteketeza juu ya mazabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa inayokuwa juu ya kuni. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.


Atawaleta kwa kuhani, naye kuhani atamutoa mumoja akuwe sadaka kwa ajili ya zambi kwa kumukongonyoa shingo yake bila kuachanisha kichwa chake.


Unga huo utachanganywa na mafuta na kupikwa juu ya kikaango. Kisha utauleta ukiwa vipandevipande na kumutolea Yawe na harufu ya sadaka yake itamupendeza Mungu.


Kisha kusafisha matumbotumbo na miguu kwa maji, Musa akaviteketeza vyote juu ya mazabahu pamoja na sehemu zingine za huyo kondoo kama sadaka ya kuteketezwa. Hiyo ni sadaka inayotolewa kwa moto, yenye harufu ya kumupendeza Yawe. Musa akafanya kama vile alivyoamuriwa na Yawe.


Kisha wakamuletea sadaka ya kuteketezwa, kipande kimojakimoja, na kichwa, naye akaviteketeza juu ya mazabahu.


mukinitolea mimi Yawe sadaka kutoka katika mifugo yenu, sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kutimiza kiapo au kutoa sadaka ya mapenzi au sadaka ya wakati wa sikukuu zenu zilizowekwa, na kufanya harufu nzuri ya kunipendeza mimi Yawe,


Wakati wa magaribi utamutoa yule mwana-kondoo mwingine kwa kuteketezwa kwa moto, pamoja na sadaka zile za ngano na za kinywaji. Itakuwa sadaka yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.


Lakini Yesu, akalalamika tena kwa sauti kubwa na kukata roho.


Wakati Yesu alipokwisha kumeza ile divai, akasema: “Yote yametimilika!” Kisha akainamisha kichwa na kukata roho.


Alitolewa kufa sababu ya makosa yetu na kufufuliwa kusudi tupate kuhesabiwa haki mbele ya Mungu.


Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ