Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Wafilipi 4:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Musijisumbue juu ya neno lolote, lakini katika kila neno mutoe mahitaji yenu kwa Mungu, mukimwomba, mukimusihi na kumushukuru.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Wafilipi 4:6
45 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, ee Yawe, Mungu wangu, unigeukie mimi mutumishi wako ninapokuomba na kukusihi. Usikilize malalamiko na maombi ambayo mimi mutumishi wako ninaomba leo.


Halafu mufalme Hezekia na nabii Isaya, mwana wa Amozi, wakamwomba Mungu na kumulilia awasaidie kwa ajili ya mambo haya.


Halafu nitawafundisha wakosaji njia zako, nao wenye zambi watarudi kwako.


Lakini mimi ninamulilia Mungu, naye Yawe ataniokoa.


Maneno yake ni matamu kuliko maziwa, lakini mawazo yake ni ya kufanya vita. Maneno yake ni laini kama mafuta, lakini yanakata kama upanga mukali.


Wokovu na utukufu wangu vinatoka kwa Mungu; kikingio changu chenye nguvu na kimbilio langu ni Mungu.


Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.


Tegemea Yawe katika kazi yako, nayo mipango yako itafanikiwa.


Ee njiwa yangu, uliyejificha katika matundu kwenye mulima, uniache kuona uso wako na kusikia sauti yako, maana sauti yako ni nzuri na uso wako unapendeza.


Kisha kumupatia Baruku mwana wa Neria barua ya ununuzi wa shamba, nilimwomba Yawe nikisema:


Uniite, nami nitakujibu na kukuambia mambo makubwa yaliyofichwa ambayo haujapata kuyajua.


Sadiraki, Mesaki na Abedenego wakamujibu mufalme: Ee Nebukadneza, sisi hatuhitaji kukujibu juu ya jambo hilo.


Hivyo, mufalme Dario akatia sahihi kwenye sheria hiyo.


Lakini watakapowapeleka kwa kuhukumiwa, musijihangaishe juu ya maneno mutakayoyasema wala juu ya namna mutakavyosema, kwa maana saa ile ile mutapewa maneno mutakayoyasema.


Pahali zile mbegu zilipoanguka katika miiba, ni mufano wa wale wanaosikia Neno la Mungu, lakini masumbuko ya dunia hii na udanganyifu wa mali vinasonga lile neno linalokuwa ndani yao na kulizuiza kuzaa matunda.


Basi musijisumbue kwa ajili ya kesho, kwa maana kesho itajisumbukia yenyewe. Kila siku ina masumbuko yake inayoitoshelea.


Basi musifanye kama wao, musifanane nao kwa maana Baba yenu anajua vitu munavyohitaji mbele hamujamwomba.


Bwana akamujibu: “Marta! Marta! Kwa nini unahangaika na kusumbuka kwa ajili ya vitu vingi?


Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ni kwa sababu hii ninawaambia: musijisumbue kwa ajili ya maisha yenu, kwamba mutakula nini; wala musijisumbue kwa ajili ya miili yenu, kwamba mutavaa nini.


Basi musijisumbue kwa kutafuta chakula au kinywaji.


Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake mufano huu kwa kuwaonyesha kwamba wanapaswa kuomba siku zote pasipo kuchoka.


Basi, Mungu hatawapatia haki wale wachaguliwa wake wanaomulilia usiku na muchana? Au atakawia kuwasaidia?


Ikiwa ulikuwa mutumwa wakati Mungu alipokuita, usihuzunike. Lakini ikiwa kuna bahati ya kupata uhuru, usiipoteze bure.


Ningependa muishi bila masumbuko yoyote. Mutu asiyeoa anashugulikia mambo ya Bwana, anatafuta jinsi ya kumupendeza Bwana.


nanyi wenyewe mutatusaidia kwa njia ya maombi. Kwa hivi Mungu atajibu kwa maombi yaliyotolewa na watu wengi kwa ajili yetu na kututendea wema, na watu wengi watamushukuru kwa ajili yetu.


Mumushukuru Mungu Baba siku zote kwa kila jambo, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.


Mumwombe Mungu kila wakati mukiongozwa na Roho. Mumwombe na kumusihi kwa kila namna. Kwa hiyo mukeshe bila kuchoka mukiwaombea watu wote wa Mungu.


Amani ya Kristo itawale katika mioyo yenu; maana ni kwa ajili ya hiyo ninyi mumeitwa kuwa katika mwili mumoja. Mukuwe wenye shukrani.


Kila kitu munachofanya au kusema, mufanye yote kwa jina la Bwana Yesu, kwa kumushukuru Mungu Baba kwa njia yake.


Mudumu katika kuomba. Munapoomba mukeshe na kumutolea Mungu shukrani.


Mbele ya yote, ninawaonya ninyi kuwaombea watu wote. Muombe Mungu awasaidie na kuwabariki, na mumushukuru kwa ajili yao.


Mujane wa kweli asiyekuwa na mutu yeyote wa kumusaidia, anamutumainia Mungu, na kudumu kumutolea mahitaji yake na kumwomba muchana na usiku.


Mwisho wa vitu vyote unakaribia kutimia. Kwa hiyo mukuwe wenye akili na waangalifu, kusudi mukuwe na uwezo wa kuomba.


Mumutolee masumbuko yenu yote kwa maana yeye anawashugulikia.


Lakini Hana akamujibu: “Sivyo bwana wangu. Mimi ni mwanamuke mwenye taabu sana; mimi sijakunywa divai wala kinywaji kikali, lakini nimekuwa nikimutolea Yawe yanayokuwa ndani ya roho yangu.


Sasa, Daudi alikuwa katika matatizo makubwa kwa sababu watu wake walikuwa na uchungu katika roho zao kwa kupoteza watoto wao. Kwa hiyo wakakuwa wakitaka kumupiga mawe. Lakini Daudi alijipa moyo kwa kumutegemea Yawe, Mungu wake.


Kisha, Samweli alitwaa jiwe na kulisimamisha kati ya Misipa na Seni, akaliita jiwe hilo “jiwe la musaada”, akisema: “Yawe ametusaidia mpaka sasa.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ