Hata hivyo, ee Yawe, Mungu wangu, unigeukie mimi mutumishi wako ninapokuomba na kukusihi. Usikilize malalamiko na maombi ambayo mimi mutumishi wako ninaomba leo.
Ee njiwa yangu, uliyejificha katika matundu kwenye mulima, uniache kuona uso wako na kusikia sauti yako, maana sauti yako ni nzuri na uso wako unapendeza.
Lakini watakapowapeleka kwa kuhukumiwa, musijihangaishe juu ya maneno mutakayoyasema wala juu ya namna mutakavyosema, kwa maana saa ile ile mutapewa maneno mutakayoyasema.
Pahali zile mbegu zilipoanguka katika miiba, ni mufano wa wale wanaosikia Neno la Mungu, lakini masumbuko ya dunia hii na udanganyifu wa mali vinasonga lile neno linalokuwa ndani yao na kulizuiza kuzaa matunda.
Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ni kwa sababu hii ninawaambia: musijisumbue kwa ajili ya maisha yenu, kwamba mutakula nini; wala musijisumbue kwa ajili ya miili yenu, kwamba mutavaa nini.
nanyi wenyewe mutatusaidia kwa njia ya maombi. Kwa hivi Mungu atajibu kwa maombi yaliyotolewa na watu wengi kwa ajili yetu na kututendea wema, na watu wengi watamushukuru kwa ajili yetu.
Lakini Hana akamujibu: “Sivyo bwana wangu. Mimi ni mwanamuke mwenye taabu sana; mimi sijakunywa divai wala kinywaji kikali, lakini nimekuwa nikimutolea Yawe yanayokuwa ndani ya roho yangu.
Sasa, Daudi alikuwa katika matatizo makubwa kwa sababu watu wake walikuwa na uchungu katika roho zao kwa kupoteza watoto wao. Kwa hiyo wakakuwa wakitaka kumupiga mawe. Lakini Daudi alijipa moyo kwa kumutegemea Yawe, Mungu wake.