22 Watu wote wa Mungu, na hasa zaidi wale wanaokuwa katika nyumba ya Mufalme, wanawasalimia vilevile.
Na kama mukiwasalimia wandugu zenu tu, munatenda tendo gani la kupita wengine? Hata wapagani wanatendeana vile!
Walihuzunika zaidi kwa sababu aliwaambia kwamba hawatamwona tena. Wakamusindikiza mpaka kwenye chombo.
Anania akajibu: “Bwana, nimekwisha kusikia watu wengi wakisema habari za mutu huyo, wakieleza mabaya aliyowatendea watu wako watakatifu wanaokuwa Yerusalema.
Musalimiane kwa upendo wa kikristo. Makanisa yote ya Kristo yanawasalimia.
Tunawatakia ninyi wote neema kutoka kwa Bwana Yesu Kristo, na upendo wa Mungu na ushirika wa Roho Mutakatifu.
Kutokana na hayo, walinzi wote wa nyumba ya mufalme pamoja na wengine wote, wanajua kwamba niko katika kifungo kwa sababu ninamutumikia Kristo.
Muwasalimie waongozi wenu wote na watu wote wa Mungu. Wandugu wa Italia wanawasalimia.
Kanisa linalokuwa katika Babeli, lililochaguliwa na Mungu kama vile ninyi, linawasalimia. Vilevile Marko, mwana wangu katika imani, anawasalimia.
Ninatumaini kwamba nitakuona sasa hivi na wakati ule tutasemezana pamoja uso kwa uso.