yeye anayekuwa Mungu peke yake, Mwokozi wetu, asifiwe na kuwa na ukubwa, uwezo na mamlaka, kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu, tangia zamani za kale, sasa na hata milele! Amina.
Na saa ile ile, kukatokea tetemeko kubwa la inchi, na sehemu moja ya kumi ya muji ikabomoka, na watu elfu saba wakakufa katika tetemeko lile. Watu waliobaki wakashikwa na hofu, nao wakamutukuza Mungu wa mbinguni.
Halafu akasema kwa sauti kubwa: “Mumuheshimu Mungu na kumutukuza, kwa sababu saa yake ya kuwahukumu watu imetimia. Mumwabudu yule aliyeumba mbingu na dunia, bahari na chemichemi za maji.”