Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Wafilipi 4:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Lakini, mumefanya vizuri kwa kushirikiana pamoja nami katika taabu yangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Wafilipi 4:14
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Yawe alimwambia baba yangu Daudi: ‘Ni vizuri kwamba ulikusudia ndani ya moyo wako kunijengea nyumba.


Lakini Yawe alimwambia baba yangu Daudi: ‘Ni vizuri kwamba ulikusudia ndani ya moyo wako kunijengea nyumba.


Bwana wake akamwambia: ‘Ni vizuri, wewe mutumishi mwema na mwaminifu. Ulikuwa mwaminifu katika ulinzi wa mali ndogo, basi nitakuweka kuwa mulinzi wa mali mengi. Kuja ufurahi pamoja na bwana wako.’


Ndiyo wamefanya vile kwa mapenzi yao, lakini vilevile ilikuwa mapaswa kwao kuwasaidia. Kwa maana ikiwa watu wa mataifa wameshirikiana baraka za kiroho na Wayuda, imewapasa watu wa mataifa mengine kuwasaidia Wayuda katika mahitaji ya kimwili.


Mwenye kufundishwa Habari Njema anapaswa kushirikiana mapato yake na yule anayemufundisha.


Ni haki kwangu kuwa na mafikiri haya kwa ajili yenu ninyi wote, kwa sababu ninawakumbuka kila mara. Kwa maana mumeshiriki pamoja nami katika neema ile Mungu aliyonipatia, ingawa sasa niko katika kifungo hata na wakati nilipokuwa huru kutetea na kuimarisha Habari Njema.


Kweli nina vitu vyote vya lazima na zaidi kupita. Sasa kwa kuwa Epafrodito ameniletea zawadi zenu zote, ninatosheka. Zawadi hizi ni kama sadaka ya ubani yenye harufu nzuri, na kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto inayokubaliwa na Mungu na kumupendeza.


Uwaagize watende mema, wakuwe watajiri katika matendo mazuri, nao wasaidiane kwa moyo safi na kushiriki mali yao na wengine.


Kwa ngambo moja mulitukanwa na kuteswa waziwazi mbele ya watu. Na kwa ngambo ingine mulishirikiana na wale waliotendewa vibaya.


Muliwahurumia wale waliokuwa katika kifungo, nanyi mulikubali kwa furaha kunyanganywa mali zenu, kwa sababu mulijua kwamba muko na mali inayokuwa bora zaidi na yenye kudumu.


Tena, musisahau kutenda mema na kusaidiana, maana sadaka za namna hii zinamupendeza Mungu.


Mimi ni ndugu yenu Yoane. Kwa njia ya kuungana na Yesu, ninashirikiana nanyi katika mateso, katika ufalme wake na katika kuvumilia. Mimi nilikuwa nimepelekwa katika kisanga kinachoitwa Patimo, kwa sababu nilihubiri Neno la Mungu na ukweli ulioshuhudiwa na Yesu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ