Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Wafilipi 3:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Nilitahiriwa nilipokuwa na umri wa siku nane. Mimi ni Mwisraeli, wa kabila la Benjamina, Mwebrania wa asili kabisa. Kuelekea mambo ya Sheria ya Kiyuda, nilikuwa Mufarisayo,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Wafilipi 3:5
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutu mumoja aliyeponyoka, akakwenda kumwarifu Abramu Mwebrania ambaye alikuwa anaishi karibu na mielo ya Mamure Mwamori. Mamure alikuwa ndugu ya Eskoli na Aneri. Wote walikuwa wamefanya agano na Abramu.


Kila mutoto mwanaume kati yenu anapaswa kutahiriwa kwa umri wa siku nane. Vilevile watumwa waliozaliwa katika nyumba yenu au walionunuliwa kwa feza zenu kutoka kwa wageni wasiokuwa wa uzao wenu. Hiki ni kitambulisho cha agano langu katika miili yenu, agano la milele.


Maana mimi nilitoroshwa kutoka inchi ya Waebrania na hapa Misri sijafanya kitu chochote kinachostahili nitiwe katika kifungo.”


Basi, kijana mumoja Mwebrania, mutumishi wa jemadari wa waaskari walinzi, alikuwa pamoja nasi katika kifungo. Tulipomwelezea ndoto zetu, yeye aliweza kutuelezea kila mumoja wetu kulingana na ndoto yake.


Yona akawajibu: Mimi ni Mwebrania; ninamwabudu Yawe, Mungu wa mbingu, muumba wa bahari na inchi kavu.


Ilipotimia siku nane tangu mutoto alipozaliwa, wakaenda kumutahiri, nao wakataka kumupa jina la baba yake Zakaria.


Ilipotimia siku ya kumutahiri mutoto, ndiyo siku ya nane tangu alipozaliwa, wakamupa jina lake Yesu. Jina hili ni lile malaika alilojulisha mbele mama yake hajabeba mimba.


Lakini inafaa kutia divai mupya ndani ya machupa mapya ya ngozi.


“Mimi ni Muyuda, nimezaliwa Tarso, katika jimbo la Kilikia, lakini nililelewa katika muji huu wa Yerusalema. Mimi nilikuwa mwanafunzi wa Gamalieli, na alinifundisha namna ya kufuata kabisa Sheria ya babu zetu. Nikajitolea kabisa kwa kutumikia Mungu kama vile ninyi wote munavyofanya leo.


Halafu Paulo alikuwa akijua kwamba watu wamoja katika Baraza Kubwa walikuwa Wasadukayo na wengine Wafarisayo. Kwa hiyo akasema kwa sauti katika baraza: “Wandugu zangu, mimi ni Mufarisayo, mwana wa Mufarisayo. Mimi ninahukumiwa kwa sababu ninatumaini kwamba wafu watafufuka.”


Katika siku zile, kufuatana na jinsi hesabu ya wanafunzi wa Yesu ilivyokuwa ikizidi kuongezeka, kulitokea manunguniko kati ya Wayuda waliosema Kigriki na Wayuda waliosema Kiebrania. Wale waliosema Kigriki walinungunika kwa sababu wajane wao walisahauliwa wakati wa kugawanya vifaa vya kila siku.


Basi ninauliza: Mungu amewatupilia watu wake? Hapana hata kidogo! Maana kwa ngambo yangu, mimi ni Mwisraeli wa uzao wa Abrahamu, toka kabila la Benjamina.


Watu wale ni Waebrania? Mimi vilevile. Wao ni Waisraeli? Mimi vilevile. Wao ni wa uzao wa Abrahamu? Mimi vilevile.


Wafilistini waliposikia sauti hiyo ya furaha walisema: “Kelele hiyo yote katika kambi ya Waebrania ina maana gani?” Walipojua kwamba Sanduku la Agano la Yawe lilikuwa limefika katika kambi ya Waisraeli,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ